Saturday, February 23, 2019

KUTAMBULISHWA, KUJITAMBUA, KUJITAMBULISHA :: [VIII] MATAMSHI YA KUJITAMBULISHA

Kama tulivyoona kujitambulisha inatokana na kutambulishwa na maandiko, kisha kujitambua.  Huu ni mzunguko ambao unatakiwa uwepo wakati wote.  Lengo lako la kwanza unaposoma maandiko ya Agano jipya hasa Nyaraka iwe ni kuona Mungu amekutambulishaje.  Baada ya hapo anza kutafakari au kufikiria kwa kurudia rudia jinsi ulivyotambulishwa, pasipo kuona ni vipi utashangaa unajitambua. Kisha anza kujitambulisha kwa kujitangaza, fanya hivi maisha yote.
Usomapo maandiko lengo liwe ni kupata maandiko ya maeneo yafuatayo, kisha tengeneza mfumo wako binafsi wa kujitambua na kujitambulisha kama ulivyotambulishwa:
Mwenye Haki Katika Yesu
Kuzaliwa Mara ya Pili
Kufa, Kufufuka, Kuketishwa na Yesu
Kazi ya Damu ya Yesu
Ukuu wa Yesu
Kuharibiwa kwa Shetani
Kuharibiwa kwa dhambi
Kuharibiwa kwa Magonjwa
Wewe na Kristo
Kristo ni Nani kwako
Wewe ni nani katika Yesu
Na Mengineyo

Unaweza angalia mfumo nilioonyesha katika kitabu hiki hasa sura mbili za mwisho na kuutumia lakini ni vema ufanye kwa jinsi yako.

No comments:

Post a Comment