Huu ni mwendelezo wa sura ya tano [V], tokea wiki iliyopita...
YESU ALIFANYA NINI MBELE ZA MUNGU KWAAJILI YAKO
Alifungua Mlango wa
Ushirika na Mungu
Angalia maandiko haya:
“6Kwa sababu Mungu ni
mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;
(1Timoteo 5:6).
“9Basi zaidi sana
tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye.”
(Warumi 5:9).
Kwa kusoma maandiko haya unajitambua jitambulishe kuwa
yanakusema wewe, hapo asemapo, “Mpatanishi
kati ya Mungu na wanadamu,jitambue na kusema jina lako au wewe”. Andiko la pili asemapo “basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki” Sema “zaidi sana
nikiisha kuhesabiwa haki” fanya hivyo kwa kutamka na kujisema, kuwaza
hivyo, utajitambua hivyo. Si maandiko haya tu, ongezea na mengine.
YESU ALIFANYA NINI MBELE ZA SHETANI
KWAAJILI YAKO
Alimharibu
“14Basi, kwa kuwa
watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo,
ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani Ibilisi,
15awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mautiwalikuwa
katika hali ya utumwa. 16 Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa
asili ya mzao wa Ibrahimu.” (Waebrania 2:14-16).
Maandiko haya kwa ujumla yanakufanya ujitambue kuwa Yesu
alikuja kama binadamu ili kwa kupitia ubinadamu kama wako amharibu shetani,
mwenye nguvu za mauti, alimharibu kwa kifo chake msalabani, katika mwili kama
wako. Shetani aliingia duniani kupitia mwili wa Adamu, Mungu amemuharibu
kupitia mwili wa Yesu.
Alimfanya si Kitu
“15akiisha kuzivua enzi
na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba
huo.” (Wakolosai 2:15).
Maandiko haya yanasema,
Yesu msalabani alizivua enzi na mamlaka.
Kuzivua kwa tafsiri ya Kiyunani ni “Katargeo”, maana yake ni; kuzifanya sio kitu,
kuzifanya sifuri,kuzipoozesha na kuzinyang’anya silaha. Jitambue kwa kujua Shetani kwako mamefanywa
si kitu, amenyang’anywa silaha zote.
Wewe ndiye mwenye nguvu juu yake kwa njia ya Yesu.
Yesu alisema, “31Sasa
hukumu ya ulimwengu huu ipo; sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.” (Yohana
12:31). Mkuu wa ulimwengu huu,
anayetajwa hapa ni Shetani. Kutupwa nje
kwake ni kunyang’anywa mamlaka na Yesu pale msalabani, na kufanywa si kitu,
kisha Yesu mwenyewe kuingia duniani na kutawala, akisema, “28…Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”
(Mathayo 28:18). Katika yeye unayo
mamlaka juu ya Shetani, jitambue hivyo.
UNA KITU GANI KATIKA YESU
Yesu alipofufuka katika wafu na kuketi mkono wa kuume wa
Mungu alirithishwa kila kitu na Baba.
Tunapompa Yesu maisha yetu tunafanywa warithi pamoja naye. Kitu chochote alicho nacho Yesu unakuwa si
sehemu ya kitu hicho, “16Roho Mwenye we
hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; 17na kama tu
watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam,
tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.” (Warumi
8:16-17).
Unalo Jina
Angalia hiki ni kitu kimoja wapo ambacho Yesu amekirithi, “14amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri
jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.” (Waebrania 1:14). Yesu
amerithi jina lililo kuu kuliko majina yote.
Inaonekana katika uungu lilikuwepo jina ambalo ilipaswa apewe mtu fulani
aliye sitahili, huyu ni yule atakaye sulubiwa na kufufuka katika wafu kisha
kuketi mkono wa kuume wa Mungu. Jina la
Yesu ni kitambulisho cha mamlaka ya Kristo.
Ukiwa nalo ni ishara katika roho ya Kristo aliyetukuzwa uliye naye. Kama vile vitu vyote vimetiishwa kwa Kristo
Yesu, vitu vyote vimetiishwa chini yako kwa jina la Yesu ulilonalo.
Yesu alipokufa tulikufa naye, alipofufuka tulifufuka naye,
alipoketi mkono wa kuume tuliketi naye, kwa kusema hivi aliporithishwa jina
tulirithishwa naye. Jitambue mahali ulipo katika ulikwengu wa roho pako hivi. Imeandikwa,
“4Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa
rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; 5hata wakati ule tulipokuwa wafu
kwasababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, mmeokolewa kwa
neema. 6Akatufufua pamoja naye,
akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu.”
Waefeso 2:4-6). Maandiko haya yanaposema alitufufua pamoja naye, kwa upande
mwingine yanaonyesha kabla hatujafufuka pamoja naye tulikufa pamoja naye. Tumeketishwa Yesu alipo tukiwa na kila kitu
alicho nacho Yesu mbele yetu, “On our disposal”. Jifikirie hivi jitambue hivi.
Unayo Haki
Ni vitu vingi tunavyo kwa njia ya Yesu Kristo siwezi viandika
vyote na kuvichambua kimoja kimoja kwa sasa, ila kipengele hiki ni moja ya mabo
ya muhimu kuyafahamu katika wokovu. Haki ni kipawa au zawadi tuliyopewa baada
ya kumwamini Yesu. Kuhesabiwa kwa njia
ya imani katika Yesu, ni kuwa sawa na Mungu katika haki yake bila kosa lolote
kwasababu tu umeiweka imani yako ndani ya Yesu.
Imeandikwa, “16hali tukijua ya
kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo
Yesu; sisi tuliomwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo,
wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili
atakaye hesabiwa haki.” (Wagalatia 2:16).
Ndiko lingine linaloongoza kuhesabiwa haki ni kipawa linasema, “17Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti
ilitawala kwasababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na
kile kipawa cha haki, watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo.”
(Warumi 5:17).
Kufahamu unayo haki kwa Mungu kwasababu ya imani yako kwa
Yesu ni msingi mzuri wa maisha ya imani yenye ujasiri bila kusikia hatia. Shetani ni mshitaki, anaweza kukosoa na kukumbusha
makosa yako, akifanya hivi kumbuka Yesu hakukosea, na wewe umeweka imani yako
kwake, Mungu anakuona huna makosa katika Yesu.
Siku zote tambua wewe umekuwa na haki ya Yesu kwa njia ya imani yako
ndani ya Yesu, si wewe peke yako.
Angalia andiko hili, “19Kwasababu
kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye
dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali
ya wenye haki.” (Warumi 5:19). Kwa kuasi kwa Adamu wote tuliambukizwa hali
ya wenye dhambi, kwa kutii kwa Yesu, wote tunaambukizwa hali ya wenye haki
wasio na dhambi kwa njia ya imani zetu kwake. Tumezaliwa kimwili na Adamu
tukawa wenye dhambi. Tumezaliwa kiroho na Yesu kwa Roho tukawa wenye haki,
jitambue hivi.
Mbingu zitatoweka kama moshi, nchi itachakaa kama vazi, ila
wokovu ulio nao katika Yesu hauchakani ni wa milele, haki yako katika Yesu
haichakai haitanguki, “6Inueni macho yenu
mbinguni mkaitazame nchi chini; maana mbingu zitatoweka kama moshi, na nchi
itachakaa kama vazi, nao wakaao ndani yake watakufa kadhalika; bali wokovu
wangu utakuwa wa milele, na haki yangu haitatanguka.” (Isaya 51:6).
WEWE NI NANI KATIKA YESU
Katika Kristo wewe ni mtoto wa Ibrahim, Yote Mungu
aliyomuahidi Ibrahimu kwa njia ya Mzao yaani Yesu ni ya kwako, hizi ni ahadi za
maongezeko, “29Na kama ninyi ni wa
Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.”
(Wagalati 3:29).
Katika Kristo wewe ni mwana wa Mungu, umezaliwa na Mungu,
unavinasaba vya Mungu, umezaliwa kwa Roho Mtakatifu, wewe na Roho Mnafanana
ndani yako, “12Bali wote waliompokea
aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake. 13
Waliozaliwa , si kwa damu wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya
mtu, bali kwa Mungu.” (Yohana 1:12-13).
Umekuwa mwana wa Mungu kwa kuzaliwa kwa njia ya imani katika
Yesu Kristo, “26Kwa kuwa ninyi nyote
mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.” (Wagalatia
3:26). Tena imeandikwa, “6Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na
kilichozaliwa kwa Roho ni roho.” (Yohana 3:6). Mwili wa nje umezaliwa na
mwili wa kibinadamu upo kama mwili wa mtu.
Roho ya ndani imezaliwa kwa Roho Mtakatifu, ipo kama Roho! Hivyo ndivyo
ulivyo katika Yesu, baada ya kumwamini!
YESU NI NANI NDANI YAKO
Kuna maandiko lukuki yanayoonyesha Yesu ni nani ndani
yako. Kumfahamu Yesu kwa ujumla, katika
hali ya ukuu wake ni mlango mkubwa wa
kumjua yukoje ndani yako. Ukisoma Ufunuo
wa Yohana kwa mfano mlango wa kwanza mpaka wa tano utaona jinzi Yesu
alivyojitambulisha katika ukuu wake.
Huyo ndiye aliye ndani yako, yakupasa ujitambue hivyo. Pamoja na maandiko mengine andiko hili
linaweza kufanya ujitambue aliye ndani yako yukoje, “4Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu; nanyi mmewashinda, kwasababu
yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko aliye katika dunia.” (1Yohana 4:4). Vyovyote alivyo Shetani, au chochote afanyacho
duniani, Yesu aliye ndani yako ni mkuu.
Kujitambua kwa namna hii kutakufanya ushinde mara zote!
Angalia Yesu aliye ndani yako jinsi alivyo, imeandikwa, “22Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda
zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.”
(1Petro 3:22). Malaika wote wa mbinguni, wa duniani na malaika waovu wa kuzimu
wako chini ya Yesu Kristo, baada ya kufufuka katika wafu na kuketi mkono wa
kuume mbinguni kila kiumbe kimewekwa chini yake! Habari njema ni kwamba Yesu
hayuko mbinguni tu, yupo ndani yako kwa hali ileile aliyonayo mbinguni. Tena imeandikwa, “1Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo
aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. 2Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo
katika nchi.” (Wakolosai 3:1-2).
Yesu alipo baada ya kufufuka katika wafu na wewe upo hapo
hapo. Ingawa upo duniani lakini kiroho
upo na Yesu mkono wa kuume. Hivyo ifikirie zaidi hali ya Yesu aliyonayo, ambayo
na wewe unayo pamoja naye na si mambo yanayokuzunguka na kukutatiza ya
duniani. Unachofikiria sana ndicho
kinachokuwa sehemu yako. Usiruhusu
kutafakari yanayokuzunguka duniani, tafakari yanayokuzunguka mbinguni, mkono wa
kuume ukiwa pamoja na Yesu. Utafakari huu utakupa kuzidi kujitambua wewe ni
nani katika Yesu Kristo. Yafikiri sana mambo haya, utakaa katika haya, kisha
mwenendo wako au tabia yako itaathirika vizuri utakuwa kama unavyoona ndani
yako, “15Uyatafakari hayo; ukae katika
hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote.” (1Timoteo
4:15). Unavyojitafakari ndivyo
unavyojitambua. Utambulisho wako wa ndani unaendana sana na nini unakifikiria
wakati wote, hali hii inaweza athiri tabia yako ya nje, jinsi unavyojiona na
jinsi unavyoonekana.
No comments:
Post a Comment