Kufikiria Kunazuia
(Reasoning Limits)
Mungu hajatuzuia kutumia fikra
zetu ametuumba nazo, Ila zinapaswa kufanywa upya zisiwe ni kikwazo cha
kushirikiana naye (Warumi 12:1-2).
Si kila kitu cha kufikiria,
visivyowezekana hatutakiwi kufikiria tunatakiwa kuamini.
Fikira zinafanya kazi na muda,
mazingira na uzoefu hali ilivyo au tuseme hali ikoje kwa watu wote. Kwa kwa
mfano kwa watu wote huwezi kupata kazi bila usaili, ila kwa Mungu unaweza
kupata bila usaili.
MIFANO YA FIKIRA
ZILIVYOKUWA KIKWAZO
1. Sina Mtu (Yohana 5:1-8)
A. Yesu alimuuliza mtu huyu,
“Wataka kuwa mzima?” Ilipasa kujibu ndio au hapana. Yeye alisema hana mtu wa
kumtumbukiza katika birika la maji ili apone, hiki kilikuwa ni kikwazo,
kufikiria hivi.
B. Yesu alitenda kinyume na fikra
zake, “Inuka Jitwike godoro uende”
TENDO:Jitwike Godoro
2. Najua Atafufuka (Yohana 11:24)
A. Yesu alimwambia Matha ndugu
yake atafufuka
B. Katika fikra zake Matha alijua
atafufuka siku ya mwisho, Pia ananuka ameshakufa siku nne (11:39), Msitari wa
21 na 22 inaonyesha pia alikuwa na anajua kwamba Yesu akiomba Mungu atajibu
(Mental agreement not faith), maana mbele alianza kusema ananuka na atafufuka
siku ya mwisho.
C. Yesu hapohapo akasema yeye ni
ufufuo na uzima, Pia akiamini ataona utukufu (11:25, 11:40)
TENDO: Liondoeni Jiwe (11:39-41)
3. Lakini Hivi ni Nini kwa Watu Wengi kama Hawa? (Yohana 6:1-9)
A. Yupo mtoto hapa na samaki
wawili na mikate mitano
B. Hivi ni nini (fikira
zinakataa)
TENDO: Waketisheni chini (10),
Akashukuru, Wagawieni(11), (Inawezekana aliposhukuru iliongezeka au alipoanza
kugawa).
4. Tumefanya kazi ya Kuchosha (Luka 5:1-5)
A. Alisema tumefanya kazi ya
kuchosha usiku kucha.
B. Hapo hapo akabadilisha na
kuingia rohoni, lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.
-Tubadilike haraka kutoka katika
kufikiria kwenda katika imani
TENDO: Tweka mpaka kilindini
5. Mimi ni mzee na mke wangu Ana umri mkubwa (Luka 1:18)
A. Zakaria na Elizabeti walikuwa
ni wenye haki (Msitari 6)
B.Elizabeti alikuwa tasa (Msitari
7)
C. Malaika aliwatokea (Msitari
11)
D. Malaika alimwambia Zakaria
maombi yake yamesikiwa, atapata mtoto wa kiume na atakuwa na furaha (Zekaria)
E. Atajazwa Roho toka tumboni,
atakuwa mkuu, atakuwa na roho ya Elia
Fikra za kuangalia muda na
mazingira zilizuia yote haya (Msitari 18).
6.Mbwa Wanakula makombo mezani mwa Bwana zao (Marko 8:24-28)
A. Mwanamke huyu alikataa fikira
kumwekea mpaka
B. Sababu za kufikirika za
kumfanya asipokee zilikuwepo
1.Ilipaswa watoto washibe kwanza
2.Sio sawa uponyaji wa watoto
wapewe mbwa
Hakukubali fikra hizi zimzuie.
7. Basi
akaenda na kunawa akarudi anaona (Marko 9:1-7)
A. Yesu alitema mate chini,
akatengeneza tope (none sense)
B. Akampaka kipofu machoni
TENDO: Nenda kanawe (Siloamu)
C. Mtu huyu hakufikiri kabla ya
kutenda alitenda tu!
D. Viongozi wa Kiyahudi
walifungwa na fikira (9:24-25)
E. Aliwajibu viongozi wa
Kiyahudi, mimi sijui ana dhambi au la (au alitumia matope) mimi najua nilikuwa
mgonjwa na sasa naona.
Tunahitaji Neno na
Roho Mtakatifu
No comments:
Post a Comment