Saturday, February 14, 2015

Inawezekana!



Yote Yanawezekana
Namshukuru Mungu kwa kutupa faraja ya maandiko yanayoonyesha kwamba yote yanawezekana kwake. Leo nimetafuta mistari michache ambayo naamini itaijenga imani yako ikiwa utaisoma na kuitafakari. Isome, irudie rudie na kuisema ,kisha utaanza kuona moyoni Mungu anaweza yote.
1. Mwanzo 18:14
Mungu alionyesha kwa Sara hakuna neno la kumshinda, atapata mtoto.
2.Yeremia 32:27
Mungu aliuliza kuna neno gani gumu la kumshinda? Kwa wenye mwili.
3.Ayubu 42:2
Ayubu alimsema Mungu kwamba anaweza yote na makusudi yake hayazuiliki.
4.Mathayo 3:9
Yohana mbatizaji alionyesha Mungu anao uwezo wa kugeuza mawe yawe watoto wa Ibrahim! Hii yaonyesha anaweza yote.
5.Warumi 4:21
Ibrahimu alijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.
6.Luka 1:37
Malaika alisema hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu, akimaanisha, hakuna ahadi ya Mungu isiyo na nguvu ya kujitimiza au kutimia.
7.Mathayo 19:26
Yesu alisema yote yawezekana kwa Mungu!
8.Yohana 15:5
Yesu alisema pasipo yeye hatuwezi lolote, kwa hiyo pamoja naye tunaweza yote.
9.Luka 17:20-21
Yesu alisema tukiwa na imani kama chembe ya haradali, imani inayokuwa na kusema tunaweza kuamisha mlima wala hakutakuwa na jambo lisilowezekana kwetu. Imani hii hutokea katika maombi na kufunga.
10.Marko 9:23
Yesu alisema yote yawezekana kwa aaminiye, Yote yawezekama kwa mtu aiwekaye imani yake kwa Mungu awezaye yote, anaanza kuweza kama Mungu awezavyo.
11. Marko 14:36
Yesu kabla hajasulubiwa wakati anaomba alisema Aba Baba yote yanawezekana kwako.
Unaweza Pamoja na Mungu

No comments:

Post a Comment