Friday, February 6, 2015

Baadhi ya Mikakati ya Adui




Mikakati ya Adui
Katika somo hili fupi utaenda kujifunza njia kadhaa atumiazo adui Shetani kuzuia uungu na kudumisha ‘ushetani’ katika maisha ya mtu au watu. Kuzifahamu mbinu zake (fikra zake) kunakupa uwezo wa kumpinga na kumzuia, hatimaye kuona mpango wa Mungu unadhihirika, hatukosi kuzijua fikra zake (2Wakorintho 2:11).
1. Anazuia (1 Wathesalonike 2:18)
Unapomuombea mtumishi au huduma mpinge Shetani asizuie shauri la kiungu kupitia mtumishi huyou huduma hiyo.
2. Anapotosha (2 Timoteo 4:1)
Kuna roho maalum ambazo kazi yake ni kupotosha mtu wa Mungu asifuate kweli. Hizi hufanya kazi katika fikra na mawazo. Kushindwa kwake ni kwa njia ya kujifunza neno la Mungu wakati wote, na kufanya maombezi katika fikra na mawazo ili kulindwa kwa damu ya Yesu, hasa kama mtu ni mchanga.
3. Anachelewesha (Danieli 10:13)
Mkuu wa Uajemi (Pepo) alichelewesha Danieli asipate majibu ya maombi yake. Mpaka pale malaika Mikaeli alipotumwa kumsaidia malaika Gabrieli kupeleka majibu kwa Danieli.
4. Anachochea (Matendo 16:17-22)
Hapa Shetani aliwachochea watu, ili Paulo na Sila wapate matatizo. Pepo waliyemkemea inawezekana alikuwa mkuu wa giza aliyeleta uchochezi huo katika watu wanaoonekana.
5. Anazingira (Ayubu 1:13-17)
Alimzingira Ayubu kwa mnyororo wa matatizo ili akufuru. Ayubu alishinda kwa kukaza macho yake kwa Mungu.
6. Anapooza (1 Samweli 17:10-11)
Wana wa Israeli walitokewa na Goliati na hawakuweza kufanya chochote walipooza. Mara nyingine adui huleta matatizo makubwa na kumpoozesha mtu kwa woga. Hapa litazame tatizo kwa kulipima na ukuu wa Mungu kisha lisemeshe kama Daudi alivyomsemesha Goliati.
7.Analazimisha (Marko 5:1-6)
Hapa mtu huyu alikuwa na pepo waliomlazimisha kufanya asiyoyataka na asiyo weza. Alikaa makaburini, alivunja minyororo nk. Shetani alimlazimisha Roho wa Mungu halazimishi, anashauri na kuhamasisha sio kulazimisha. Dalili za utandaji wa pepo ni mtu kufanya kwa nguvu vitu asivyotaka kufanya, au mtu kulazimisha mtu mwingine afanye jambo hasa kama ni baya. Mtu wa namna hii inawezekana anaongozwa na pepo.
8. Anapofusha (2 Wakorinto 4:4)
Kwa watu wasiookoka Shetani anawapofusha katika fikra zao wasielewe injili, Kisha wafe katika dhambi zao. Maombi ya kuwaombea ni kufunga giza la kishetani na kufungulia nuru ya Kristo waelewe injili. Kwa mtu aliyeokoka na anadumu kuendelea na dhambi atafanywa moyo mgumu na kupofushwa. Mwishowe hataweza  kutubu na atapotea milele.
HII NI BAADHI YA MIKAKATI TU YA ADUI. TUNAWEZA KUMZUIA KWA JINA LA YESU, DAMU YAKE NA NENO LA MUNGU.

No comments:

Post a Comment