Saturday, January 10, 2015

Tunayo Miliki ya Yesu na Kazi Zake


HATI MILIKI YA YESU
Jina la Yesu ni kama hati miliki ya kummiliki Yesu na kazi zake hapa duniani. Kazi ya hati ni kutoa haki na uwezo wa kumiliki ardhi, nyumba nk. Jina la Yesu limetupa uwezo sisi waumini wa kuzimiliki kazi zote alizozifanya Yesu! Pia kuwa na Yesu sasa.
Kichwa, Mwili, Matendo
(Waefeso 1:22-2)
Yesu ni kichwa cha kanisa, kanisa ni mwili wake. Mwili huwa unayo matendo fulani, mwili wa Yesu unayo matendo yake. Unayatenda matendo hayo kwa kutumia jina la Yesu. Kwa jina la Yesu kanisa limemiliki hali ya Yesu aliyonayo mkono wa kuume wa Mungu. Yuko juu ya nguvu na mamlaka zote. Udhihirisho wa hali hiyo ya nguvu na mamlaka unaonekana kwa kupitia kanisa hapa duniani kwa jina lake.
Mambo Tunayomiliki kwa Jina lake
1. Kwa jina la Yesu tunamiliki Wokovu (usalama wa milele),  (Matendo 2:21).
2. Kwa jina la Yesu tunamilliki uponyaji (Yoeli 2:32).
3.Kwa jina la Yesu tunaingia patakatifu pa patakatifu kwa njia ya kuomba kwa jina lake. Huku ni kuomba kwa kumtumia Yesu (Yohana 16:23).
4.Kwa jina la Yesu tunatenda kama alivyotenda na kazi kubwa zaidi (Yohana 14:12-13).
5.Kwa jina la Yesu tunatoa pepo kama alivyotoa (Marko 16:17).
6. Kwa jina la Yesu tumemilikishwa uwezo na mamlaka ya kuwa juu ya vyote kama Yesu alivyo (Yohana 3:35, Mathayo 11:27, Mathayo 28:18).
7. Kwa jina la Yesu tunao uwezo wa kuingia popote na kuamuru jambo litokee hata kama tuko mbali kimwili (1 Wakorintho 5:3-4).
ASANTE BABA KWA KUTUMILIKISHA YESU NA KAZI ZAKE KWA JINA LAKE

No comments:

Post a Comment