FUNGUO ZA UFALME
Ufalme wa Mungu unaonekana kwa tabia za Mungu, pia nguvu na mamlaka yake. Funguo ni ishara ya mamlaka na nguvu za Mungu.
I.
FUNGUO
Maphteah (Kiebrania)
– kifungulia (Opener)
Waamuzi 3:25 “Wakamngoja
hata wakatahayari; na tazama, hakuifungua milango ya chumba; basi wakatwaa
ufunguo, na kuifungua; na tazama, bwana wao alikuwa ameanguka nchi, naye
amekufa.”
Kleis
(Kiyunani) - Kufunga
Luka 11:52 “Ole
wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa maarifa; wenyewe
hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia.”
II.
Funguo
ni Mamlaka na nguvu (Alama ya mamlaka na nguvu)
MAENENO
ZINAPOONEKANA KIMAANDIKO
1. Begani. Isaya
22:22 “Na ufunguo wa nyumba ya Daudi
nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga
wala hapana atakayefungua.”
· Inaonyesha mtawala
aliye katika ofisi yenye mamlaka. Ofisi hii ni ya Kristo.
· Kristo ana uweza wa
kifalme begani (funguo za kifalme)
2. Petro
· Yesu alimwambia
Petro amempa funguo za Ufalme. Mathayo
16:19 “Nami nitakupa wewe funguo za
ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa
mbinguni; na lolote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
· Mamlaka na nguvu ya
kifalme
3. Yesu
· Anazo funguo za
mauti na za kuzimu. Ufunuo 1:18 “na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na
tazama, ni hai; nami hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za
kuzimu.”
· Anazo funguo za
Daudi. Ufunuo 3:7 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia
andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na
ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala
hapana afunguaye.”
· Mamlaka na nguvu ya
ufalme.
4. Malaika.
· Ufunuo 9:1 “Malaika
wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya
nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu.”
· Ufunuo 20:1 - 2 “Kisha
nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo
mkubwa mkononi mwake. (2) Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni
Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu “
5. Maarifa
· Ufunguo wa ufalme
· Kuyashiriki mambo ya
kifalme, maarifa ni uwezo na mamlaka ya kufanya hivyo.
Luka 11:52 “Ole
wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa
maarifa; wenyewe hamkuingia, na wale
waliokuwa wakiingia mmewazuia.”
· Mathayo 23:13 “Ole
wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa
mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.”
SIKU MOJA WAKATI
NAOMBA ASUBUHI NILIFAHAMU KWAMBA:
1.
FUNGUO
NI MAMLAKA YA KUTENDA.
Ufunuo 1:18 “na
aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai; nami hata milele na
milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.”
Maandiko
haya yanaonyesha:
-
Yesu
anazofunguo za mauti na za kuzimu, anayo mamlaka ya kudhibiti, mauti na kuzimu.
-
Mikononi
mwake ameshika mamlaka yote ya utendaji wa mauti (nguvu) na kuzimu (viumbe vya
kuzimu).
-
“Control”
ya utendaji wa mauti na kuzimu ipo chini yake
-
Maamuzi
ya mashetani juu ya watu ameyashika na kuyazuia
-
Hawawezi
kufanya watakavyo tena
2.
FUNGUO
NI UFUNUO WA KIROHO
Mathayo 16:16 – 19 “Simoni
Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. (17) Yesu
akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Baryona; kwa kuwa mwili na damu
havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni. (18) Nami nakuambia, Wewe
ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya
kuzimu haitalishinda. (19) Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na
lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote
utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
· Petro alipopata
ufunuo Yesu ni nani, Yesu akataja funguo
· Tupatapo ufunuo,
tayari tuna funguo, Maarifa ni funguo. Luka 11:52 “Ole wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa maarifa;
wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia.”
RHEMA NI FUNGUO
· Rhema katika
maombezi
· Rhema katika
mahubiri
· Rhema katika maisha
3. UWEZO WA KUZUIA NA
KUACHILIA
Ufunuo 3:7 “Na
kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye
mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala
hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye.”
Yesu anafungua
(Anaruhusu) wala hapana azuiaye. Anazuia (Anafunga) wala hapana anayeruhusu.
· Kwa kutumia jina
lake tunauwezo wa kuruhusu na kuzuia vitu. Marko
16:17 “ Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa
pepo; watasema kwa lugha mpya;”
· Kwa nafsi yake tuna
uwezo wa kuruhusu na kuzuia vitu. Yohana
14:30 “Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa
ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu.”
· Kwa Neno lake tuna
uwezo wa kuruhusu na kuzuia vitu Yohana
8:51 “Amin, amin, nawaambia, mtu
akilishika Neno langu, hataona mauti milele.”
· Kwa damu yake yake
tuna uwezo wa kuruhusu na kuzuia vitu. Ufunuo
12:11 “Nao wakamshinda kwa damu ya
Mwana-Kondoo, na kwa neon la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata
kufa.”
· Kwa Roho wake tuna
uwezo wa kuruhusu na kuzuia vitu. Isaya 59:19 “
UNAZO FUNGUO KATIKA
KRISTO
Soma Maandiko haya
1.
1Petro
3:22 “Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu,
amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini
yake.”
2.
Yohana
3:35 “Baba amempenda Mwana, naye amempa
vyote mkononi mwake.”
3.
Mathayo
28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao,
akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”
4.
Mathayo
11:27 “Akasema, Nimekabidhiwa vyote na
Baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana,
na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia.”
5.
Yohana
10:17 – 18 “Ndiposa Baba anipenda, kwa
sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. (18) Hakuna mtu aniondoleaye, bali
mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa
tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.”
6.
Yohana
10:30 “Mimi na Baba tu umoja.”
7.
Yohana
1:18 “Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati
wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.”
8.
Yohana
8:58 “Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia,
Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.”
9.
Ufunuo
3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko
Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu
na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.”
10.
1Petro
2:6 “Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko
Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila
amwaminiye hatataharika.”
MAMLAKA YA KUTENDA
YA SHETANI YESU AMEISHIKA
-
MAUTI
(Nguvu)
-
KUZIMU
(Mashetani)
INATHIBITIKA KWAKO
-
KWA
JINA LAKE
-
KWA
NENO LAKE
-
KWA
ROHO WAKE
-
KWA
DAMU YAKE
-
KWA
NAFSI YAKE
No comments:
Post a Comment