UNAYO MAMLAKA
Katika maandiko usomapo, hasa
Agano jipya utagundua kwamba sisi ndiyo tunayo mamlaka ya kumshughulikia
Shetani na sio Mungu. Mungu ametupa mamlaka sisi. Katika maandiko yafuatayo
utaona wajibu upo kwetu ili kumshughulikia Shetani, Mungu anatenda kupitia sisi:
1. Mtiini Mungu,
Mpingeni Shetani naye atakimbia
(Yakobo 4:7)
Andiko hili
linaonyesha ni sisi tunaompinga Shetani. Wajibu wa kumpinga na kumfukuza ni
wetu!
2. Nawapa amri,
Kukanyaga nyoka na nnge na nguvu
zote za yule mwovu (Luka 10:19)
Ni sisi waamini
ndio tunao wajibu wa kukanyaga nyoka na nnge na nguvu zote za Shetani wala
hakuna kitu kitakachotudhuru.
3. Lolote mtakalolifunga duniani litafungwa na
mbinguni (Mathayo 18:18-19)
Uwezo wa
kufunga jambo au kufungua upo katika mikono yetu.
4.Nimepewa
mamlaka yote mbinguni na duniani, enendeni
(Mathayo 28:18-19).
Yesu amepewa
mamlaka yote mbinguni na duniani, kwa mamlaka hiyo aliyo nayo sisi tunaenda
duniani kufanya jambo siyo yeye.
5. Na Ishara
hizi zitafuatana na hao waaminio kwa jina langu watatoa pepo (Marko 16:17-18).
Uwezo wa
kutoa pepo ni wetu, Ni sisi tunaotoa pepo
kwa kutumia jina alilopewa Yesu, lililobeba mamlaka yake yote.
MAANDIKO
YANASEMA YESU AMEFANYWA KICHWA JUU YA VYOTE KWAAJILI YA KANISA (WAEFESO
1:22-23), SIYO KWAAJILI YAKE. AMEWEKWA JUU YA VYOTE KWAAJILI YETU, ILI SISI
TUWEZE KUFANYA JAMBO FULANI BADALA YAKE KAMA WAWAKILISHI WAKE.
No comments:
Post a Comment