Kufanywa Mwana
“Kwa kuwa hamkupokea tena roho ya utumwa iletayo hofu; bali mlipokea
roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia Aba, yaani Baba.” (Warumi
8:15).
“Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi
pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana yaani, ukombozi wa
mwili wetu.” (Warumi 8:23).
Nyakati za Warumi na Wayunani,
ikiwa mtu hakubahatika kupata mtoto, aliruhusiwa kuwa na mtoto ambaye sio wake
kwa asili, ALIYEFANYWA MWANA, kwa kwa hatua na taratibu maalum. Mtoto huyo
alitumia jina la baba huyu mpya kama baba yake kabisa na alikuwa na haki ya
kurithi mali zake. Kitendo hiki cha kufanywa mwana
kilikuwa na ngazi kuu mbili:
1. Kutambulika mwana binafsi
2.Kutambulika mwana katika jamii
KUTAMBULIKA BINAFSI
Hapa mtoto huyu mpya aliweza kuingia
katika familia na kufanywa mwana halali. Alijulikana katika familia husika kama
mwana na mrithi. Mwandishi wa Warumi alikuwa na maana hii katika andiko
lifuatalo, “Kwa kuwa hamkupokea tena roho
ya utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo
twalia Aba yaani Baba.” (Warumi 8.15). Sisi pia, Tulifanywa wana katika
familia ya Mungu baba tukiwa hapa duniani, si wana tu tumefanywa warithi wake
kwa njia ya Yesu, tunarithi vyote alivyorithi Yesu baada ya kufufuka katika
wafu; Jina, mamlaka, haki yake nk.
KUTAMBULIKA KATIKA
JAMII
Baada ya kujulikana katika familia mtoto huyu, alitangazwa
wazi katika jamii. Hapa alitangazwa kwa
uwazi zaidi. Andiko hili lifuatalo ndilo mwandishi alikuwa ana maana hii, “Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio
na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia
kufanywa wana yaani, ukombozi wa mwili wetu.” (Warumi 8:23).
Hata sisi, Siku moja tutaonekana wazi katika ufalme wa Mungu
tutakapotambulishwa na Mungu mbinguni, baada ya miili yetu kubadilishwa na kuwa
kama Yesu, tutaurithi uzima wa milele.
IKIWA UMEMPOKEA YESU,
WEWE UMEFANYIKA MTOTO WA MUNGU. HUKUWA MTOTO ILA KWA NJIA YA YESU UMEFANYIKA
MTOTO. UMERITHI YOTE ALIYORITHISHWA YESU BAADA YA KUFUFUKA. SASA UNASUBIRI
KUTAMBULISHWA MBINGUNI KATIKA UFUFUO WA MILELE. USIKATE TAMAA, ICHUCHUMILIE
SIKU HIYO.
No comments:
Post a Comment