IV. Amani Kabla ya Anguko
Kabla
ya Adamu kumkosea Mungu katika bustani ya Edeni alikuwa na amani na
Mungu kwa sababu alikuwa na haki
na uzima.
Adamu
alipokosea alikuwa adui na Mungu-Amani hamna
Alikuwa
anamashitaka katika dhamiri yake-Amani hamna
Kabla
alikuwa na utulivu wa ndani, na kati yake na Mungu kwasababu ya
kutokuwa na dhambi, Kazi ya haki ya Mungu ndani yake ilimpa amani,
“Na
kazi ya haki itakuwa amani. Na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na
matumaini daima.”
(Isaya 32:17).
Baada
ya kumwasi Mungu Adamu alipoteza haki, hapohapo amani ikapotea,
inaonekana kuwa amani ya ndani haikuwepo ndio maana alianza
kujificha.
-Alipokosa
haki ya Mungu kwa kuasi akawa mtu mbaya na hapana amani kwa wabaya.
“Mimi
nayaumba matunda ya midomo; amani, amani kwake yeye aliye mbali na
kwake yeye aliye karibu. Bali wabaya wanafanana na bahari
iliyochafuka; maana haiwezi kutulia. Hapana amani kwa wabaya; asema
Mungu wangu.”
(Isaya 57:19-21)
*Adhabu
mojawapo aliyoipata Adamu baada ya kutenda dhambi ni kukosa amani.
V. Chanzo
cha Amani
Yesu
alikuja ili tuwe na utulivu wa ndani na kutokuwa na uadui kati yetu
na Mungu.
Alikuja
kuiondoa dhambi ya Adamu, iliyotufanya tusiwe na amani na Mungu
Pia
alikuja kutoa damu yake dhamiri zetu zisafishwe tuwe na amani ndani
yetu.
Jambo
lingine alilofanya ni kubeba adhabu ya amani aliyoipata Adamu yaani
kukosa
amani.
“…Adhabu
ya amani yetu ilikuwa juu yake na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”
(Isaya 53:5).
Pia
unaweza kusoma (Waefeso 2:15-17).
-Kazi
ya Yesu Msalabani imeleta amani na MUNGU
-Amani
Katika mioyo
-Amani
kati ya watu
Mtu
anapotubu dhambi zake kupitia Yesu, na kuitegemea kazi ya msalaba na
damu ya Yesu ili asamehewe, hupatanishwa na Mungu (HUWA NA AMANI NA
MUNGU SI UADUI), pia hatia ya dhambi huondolewa moyoni kwa damu ili
awe na utulivu kwa Roho Mtakatifu, utulivu huu ni amani.
Usikose sehemu ya Mwisho ya Somo Hili, ambapo Tutaangalia Umuhimu wa Amani katika Maisha Yetu na Funguo za Kuipata Amani. MUNGU Akubariki kwa Kuendelea Kujifunza.
No comments:
Post a Comment