Amani
ni nini?
Kunaweza kuwa na Tafsiri mbalimbali za Neno Amani, hii ni kutokana na weredi na upana wa lugha. Lakini mimi ningepedna nifupishe kwa kusema kuwa amani ni hali ya:-
-Utulivu
-Ukimya
-Kutokuwa
na mahangaiko au vurugu
-Usalama
-Kutokuwa
na uadui
“Kwa
maana Mungu si wa machafuko, bali wa amani”
(1Wakorintho
14:33)
-Mungu
si wa vurugu
-Mungu
si wa mahangaiko
-Mungu
ni wa usalama
-Mungu
ni wa upatanisho si uadui
-Mungu
ni wa amani
- Mazingira ya Kimwili na Kiroho
Wanadamu
tuko katika hali mbili kwa wakati mmoja tuko mwilini na rohoni.
Katika
hali hizi mbili ili tufanye mambo kwa ufanisi tunahitaji Amani.
- Mazingira ya kimwili
Kusipokuwa
na amani kimwili ni vigumu kuwa na mafanikio katika yale ufanyayo.
Kwa mfano kama wewe ni mfanya biashara kukiwa na vurugu mjini
utafunga duka maana hakuna amani.
Hili
ni swala la kimwili, lakini hata kiroho usipokuwa na amani utakosa
ufanisi wa kufanya jambo.
- Mazingira ya Kiroho
Usipokuwa
na utulivu wa ndani kiroho si rahisi uwe na mafanikio katika maswala
ya kiroho kama vile:
-Kumwamini
-Kumtumikia
-Kumsikia
-Kumwabudu
na kumsifu
-Kupata
uponyaji wa ndani (vidonda)
Usikose Muendelezo wa Somo hili, Kwani Tutajifunza Mambo Kadhaa kuhusu Amani, kama vile; Nini Chanzo cha Amani? Amani Kabla na Baada ya Anguko, Funguo za Amani, Kazi za Amani, nk.
Lengo ni Kuamsha Ndani Yetu Kiu na Shauku ya Kuitafuta Amani Sahihi katika Maisha Yetu.
Mtu
anapotubu dhambi zake kupitia Yesu, na kuitegemea kazi ya msalaba na
damu ya Yesu ili asamehewe, hupatanishwa na Mungu (HUWA NA AMANI NA
MUNGU SI UADUI), pia hatia ya dhambi huondolewa moyoni kwa damu ili
awe na utulivu kwa Roho Mtakatifu, utulivu huu ni amani.
No comments:
Post a Comment