Saturday, August 23, 2014

Unapochochea Imani

Piga Vita Vizuri Vya Imani



Utangulizi
Imani ni nini? Maandiko yanasema “Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo yasioonekana” (Waebrania 11:1). Andiko hili linaonyesha imani ikitafsiriwa meoneo mawili: 1. Kuwa na uhakika wa mambo yatalajiwayo  2. Bayana ya mambo yasioonekana.

Kuwa na Hakika.

Kipengele hiki cha kuwa na hakika kinahusiana na moyo. Ni kuwa na  uhakika moyoni. Tafsili halisi ya kuwa na uhakika ni “ kuwa na uhalisi”. Neno la Kiyunani linalotumika kuonyosha uhakika katika andiko hili ni “hupostasis”, ambalo linaonyesha kitu halisi ambacho kitu kingine kinajengwa juu yake, kwa mfano msingi wa nyumba ni kitu halisi ambacho myumba inajangwa juu yake. Kwa namna hiyo hiyo, imani ni msingi ni uhalisi wa moyoni wa mambo unayotarajia kutokea wazi, Yadhihirike mwilini. Imani ni uhalisi wa sasa ndani yako  wa mambo unayotarajia kuyaona nje baadaye. Imani inapokea sasa kitu ambacho hakijaonekana.
Tafsiri hii inatoka katika neon la Kiyunani “pistis”, Neno hili ni jina. Tendo lake linaitwa “pisteuo” yaani kuamini, kuamini ni kuitendea kazi imani iliyopekea sasa, mambo yatarajiwayo kuokea au kudhihirika. Imani ya moyoni hudhihirisha yaarajiwayo kutokea kwa njia ya kuamini; Kwa mfano kuomba, kushukuru, kutenda jambo lililosemwa na ahadi nk. Imani inadhihirishwa kwa kuamini, kuamini kunadhihirisha yaarajiwayo.Kabla hujaona jambo unalotarajia linatokea, lazima msingi wa jambo hilo ujengwe, unaitwa uhakika ua uhalisi wa jambo hilo sasa katika moyo.
                                   Bayana ya Yasioonekana
Imani pia inafanya kazi na mambo bayana au dhahiri yasioonekana.  Mambo hayo ni: Mungu na Neno lake.  Mungu na Neno ni dhahiri ingawa hawaonekani; ni kama vile upepo upo dhahiri / bayana lakina hauonekani.  Neno la Mungu pia ni dhahiri ingawa halionekani,  ni kama vile mawimbi ya redio, yalivyo bayana ingawa hayaonekani. Uhalisi wa ndani sasa  hujengwa na udhahiri usioonekana, yaani Mungu na Neno lake. Moyo uonapo udhahiri wa Mungu na Neno lake, kwamba yale aliyosema ni kweli na yanatimia, hujenga uhalisi /uhakika. Uhakika huu hubeba matarajio  ya kuona jambo likitimia mwilini. Kwa lugha rahisi tunaweza kusema, matarajio ya jambo kutokea kujengwa, Hujeengwa juu ya uhakika wa sasa moyoni, uhakika huu hujengwa na ubayana wa Mungu na Neno lake.  Shetani anatafuta imani aiuwe kwa hiyo yatupasa tuishindanie au tuilinde. Kulinda imani ni kupigana vita vizuri vya imani. Kwa upande mwingine Mungu huitumia imani yetu tushirikiane naye na kumpingani Shetani. Kumpinga Shetani kwa imani kwa njia ya ahadi za Mungu ni vita vya imani.
Kwa upande mwingine Mungu tunampendeza kwa imani. Ukitaka kufanya mapenzi ya Mungu kitu cha kwanza kukitafuta na kukielewa ni imani.  Maandiko yanasema pasipo imani haiwezekani kumpendeza (Waebrania 11:6).  Maandiko mengine yanasema, “Angalieni, ndugu zangu, usiwe katika mmoja wenu moyo mbovu wa kutokuamini, kwa kujitenga na Mungu aliye hai.” (Waebrania 3:12). Andiko hili linaonyesha kwamba kuwa na moyo mbovu ni kutokuamini, moyo wa namna hii ni moyo uliojitenga na Mungu!  Msitari wa 19 unasema, “Basi twaona ya kuwa hawakuweza kuingia kwasababu ya kutokuamini kwao”. Hawakuingia kwa kuasi, Kutokuamini ni kama kumwasi Mungu, watu hawa hawakuingia Kaanani kwa kutoamini, kuasi, “ Tena ni kina nani aliowaapia ya kwamba hawataingia katika raha yake, ila si wale walioasi?”(Waebrania 3:19). Yesu alionyesha kutokuamini ni dhambi, “Kwa habari ya dhambi, kwasababu hawaniamini mini;…”( Yohana 16:9). Kutokumwamini Yesu ni dhambi na ni chanzo cha dhambi zote. Kwa hiyo ni vema kuielewa imani ili kuweza kumpendeza Mungu, kuishi naye, kutokumwasi na kuingia katika ahadi zetu tulizopewa, ikiwemo ya kuingia mbinguni.
 Kitabu hiki ni toleo la pili. Toleo la kwanza liliitwa Chochea Imani Yako. Katika toleo hili kuna mambo mengi  mapya ni vyema kama ulishakisoma, kusoma upya.

No comments:

Post a Comment