Thursday, August 21, 2014

Shuhuda-Jina la Yesu 1, EV Grace Mbise


Nguvu ya Jina la Yesu
Jina la Yesu tumepewa sio kwaajili ya kuombea wagonjwa na kutoa pepo tu.  Tumepewa jina hili tulitumie katika mazingira yote tuliyo nayo.  Maandiko yanasema, “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu,…” (Wakolosai 3:17).  Katika huduma na maisha yake, mama Mbise ameonekana kulitumia jina la Yesu si katika maombi kwa wenye shida tu, bali hata katika maisha ya kila siku.  Kama anavyoshuhudia katika maneno haya:

Miaka ya tisini nilikwenda eneo la Sakila katika huduma ya ushuhuda wa nyumba kwa nyumba.  Tukaingia katika nyumba ya mzee mmoja aitwaye Mathayo.  Alikuwa na ugonjwa wa pumu ambao ulisababishwa na pepo.  Wakati tunamwombea pepo alitamka na kusema haondoki.  Karibu na mlango kulikuwa na mbwa wake.  Yule baba alikuwa amelala chini anaangalia wale mbwa wakati tunaendelea kuomba. Mara nyingine tena nikamwamuru yule pepo na kusema, “kwa jina la Yesu toka”.  Mara mbwa mmoja pale nje akakohoa kama aliyebanwa na pumu akajinyoosha na kufa.  Ghafla yule baba akainuka na kusema amefunguka.  Baba huyu aliogopa sana akasema, “jamani naomba mniombee maana kuna Mungu” (Hii ilikuwa ni ishara iliyomfungua macho mgonjwa huyu, akatambua kwamba kuna Mungu mara tu alipopona. Uponyaji huu ulikuwa ishara kwake, ishara mara nyingi ni uponyaji, muujiza au ufunuo ambao unaashiria kwamba Mungu yupo nyuma ya utendaji huo na kumvuta mtu kumwamini au kumtukuza.)  Yesu alipofanya muujiza wa kugeuza maji kuwa divai (Yohana 2:1-11), muujiza huu ulikuwa ni ishara au ufunguo kwa wanafunzi, maana walifumbuliwa macho na wakamwamini.  Mtumishi anaendelea kushuhudia kwa kusema:

Kwa kumfungua mzee huyu kutoka kwenye pumu Mungu alionyesha kwamba uhai wa mtu una thamani kuliko mnyama.  Ndio maana aliruhusu mbwa yule afe kwa kuingiliwa na pepo aliyetoka ndani ya mtu na mtu akapona.

No comments:

Post a Comment