Alimwaga Damu
toka katika Mwili
Damu
ya mnyama inabeba uhai wa mnyama huyo (Mambo ya Walawi 17:11). Kwa hiyo kumwaga
damu ni sawa na kumwaga uhai. Yesu alipotoa uhai wake maana yake mojawapo ni
kusema alitoa damu yake
(1Yohana 3:16).
(1Yohana 3:16).
Utakaso na
Ondoleo la Dhambi
Damu
ya Yesu imetolewa kwaajili ya kuondoa dhambi na kumbukumbu yake mbele za Mungu.
Pia imetolewa kusafisha dhambi katima moyo wa aaminiye hata dhamiri yake
ikaweza kusimama bila hatia mbele za Mungu. Tunaposhiriki Meza ya Bwana tukiri
kwamba kwa damu ya Yesu tunaloondoleo la dhambi. Hakuna kumbukumbu ya dhambi
zetu mbele za Mungu. Pia tukiri na kusema inatusafisha mioyo yetu na matendo
mafu, hivyo dhamiri zetu zinao ujasiri wa kusimama mbele za Mungu.
Kuokolewa na
Gadhabu kwa Damu
Kwa
njia ya damu ya Yesu tumeokolewa na ghadhabu itakayokuja (Warumi 5:9). Kwa njia
ya kuhesabiwa haki kwa damu ya Yesu tunaokolewa na ghadhabu au hasira ya Mungu
inayokuja. Ni vizuri wakati wa meza ya Bwana kukiri kwamba umeokolewa na
ghadhabu na hutaingia hukumuni.
Damu na
Kufufuliwa kwa Yesu
Yesu
alifufuka kwa Damu yake. Abili alipouwawa
damu yake ililalamika kwa kuwa aliuwawa pasipo haki (Mwanzo 4:10). Damu
ya Yesu nayo ilikuwa na cha kusema alipouwawa (Waebrania 12:24). Inawezekana
kabisa kwamba moja ya kitu ambacho damu ilinena mbele za Mungu ni haki ya Yesu.
Damu ilisema huyu aliyeuwawa hana dhambi ni mwenye haki, wenye dhambi ndio
wanaostahili kukaa kuzimu. Damu ilisema: kwa kuwa Yesu aliyeuwawa hana dhambi
bali amekufa kwa dhambi za wengine, inampasa asikae kuzimu kwa wenye dhambi.
Hii inawezekana ndiyo sababu moja wapo iliyomwezesha kufufuka (Waebrania
13:20). Tunaposhiriki meza ya Bwana tukiri na kusema katika damu ya Yesu tunazo
nguvu za ufufuo. Maeneo yote katika maisha yetu yenye dalili za kifo damu ya
Yesu inaleta ufufuo.
Damu na Kupaa kwa
Yesu
Yesu
alipofufuka alitamka maneno haya kwa Mariamu, “…Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu
zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, Kwa Mungu
wangu naye ni Mungu wenu.” (Yohana 20:17). Hapa tunamwona Yesu akikataa kushikwa
na Mariamu kwa kuwa hajaenda kwa Baba. Lakini sehemu nyingine baada ya kufufuka
alisema, “…Lete hapa kidole chako;
uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu.” (Yohana
20:27). Kwa nini msitari wa kumi na saba alimkataza Mariamu asimguse kwa kuwa
hajapaa! Na msitari wa ishirini na saba alikubali Tomaso amguse wakati bado
alikuwa hajaondoka na kupaa mbinguni! Kupaa alikokusema msitari wa 17 kulikuwa
ni nini?. Kupaa huku hakukuwa kule kwa kwenda mbinguni na kuketi mkono wa
kuume, kulikuwa ni kupaa kwaajili ya kuipeleka damu yake. Inawezekana hakutaka
aguswe kwakuwa alikuwa anaenda patakatifu pa patakatifu mbinguni kuwakilisha
kwa Baba kitu kitakatifu sana
yaani damu yake. Tunaposhiriki meza ya Bwana tutamke kuwa damu ya Yesu ipo
mbele za Mungu ikishuhudia wokovu wetu ilipelekwa na Yesu.
Damu na Ukuhani
wa Yesu Mbinguni
Kama tulivyoona sehemu iliyopita
Yesu alienda mbinguni kupeleka damu pindi tu alipofufuka. Baada ya hapo alikuwa
akiwatokea wanafunzi kwa siku arobaini. Mwisho alipaa na kuondoka duniani
akaketi mkono wa kuume mbinguni. Maandiko yanasema, “Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni,
akaketi mkono wa kuume wa Mungu.” (Marko 16:19). Yesu alimwaga damu, akafa,
kwa damu hiyo akafufuliwa. Kupitia damu aliingia kwa Mungu. Damu ya Yesu inao
ushuhuda wa Yote aliyofanya Yesu katika mwili, kama
vile damu ya Habili ilivyoshuhudia aliyofanyiwa katika mwili. Alipopaa na
kuketi mkono wa kuume ameketi akiwa na damu yake, inayosema amemshinda Shetani
kwaajili yetu, kwa kupigwa kwake tumeponywa, tumenunuliwa toka nguvu za giza, tumepata uzima wa
milele.
Yesu
mkono wa kuume wa Mungu ni mfalme mkuu. Baada ya Yeye kuketi mkono wa kuume,
Roho Mtakatifu alitolewa na Mungu Baba kuja duniani (Matendo 2:33). Roho wa
Mungu ndani ya waaminio, anawapa waamini nafasi ya Kristo katika kumiliki
nafasi ya ufalme. Anadhihirisha
kwamba wamekufa pamoja naye, wamefufuka pamoja naye na wameketishwa mkono wa
kuume na Yesu (Waefeso 2:1-6).
Yesu
mkono wa kuume wa Mungu ni kuhani wetu mkuu. Ameonekana mbele za Mungu kwaajili
yetu. Yeye ndiye aliyetupatanisha na Mungu na ni shahidi wa Agano letu na
wokovu wetu. Kwa yeye tunayoamani ya kumkaribia Mungu bila hofu, maana yupo
mbele yake kwaajili yetu, tena ndiye anayetuombea (Waebrania 9:24, Waebrania
7:25). Katika yeye tumefanywa makuhani. Tunalo
neno la upatanisho, tunasimama kati ya dunia na Mungu, kama
vile Yesu afanyavyo. Yesu alichinjwa/alisulubiwa kwa damu yake akatununua kwa
Roho wake akatufanya wafalme na makuhani mkono wa kuume wa Mungu. Katika ufalme
na ukuhani huu tunamiliki juu ya nchi (Ufunuo 5:9-10).
Haya
yote mlango wake ni damu Yesu aliyoingia nayo mbinguni. Tunaposhiriki meza ya
Bwana tuseme, kwa njia yake Yesu alienda mbinguni, akaketi mkono wa kuume,
akiwa mfalme na kuhani mkuu. Kutoka hapo akatupa Roho wa Mungu, na tumeketishwa
mbinguni pamoja naye katika Roho Mtakatifu. Juu sasa kuliko mamlaka yote, enzi,
malaika, usultani na nguvu zote.Mkono wa kuume tupo juu ya majina yote, na tuna
jina kuu kuliko yote, kama wafalme.Tunaombewa
na Yesu anayasimamia maungamo au maneno yetu mbele za Mungu (Webrania 3:1).
Tunawapatanisha watu na Mungu. Tunamwakilisha Mungu duniani katika kuwahudumia
wanadamu kama makuhani (1Petro
3:22,Waefeso1:20-22,Wafilipi 2:9-11).
Damu ya Yesu na
Mashitaka ya Shetani
Shetani
ni adui yetu yeye ni mshitaki. Anasimama mbele za Mungu kinyume na sisi. Hata
hivyo ashukuriwe Mungu kwa kuwa damu ya Yesu inasema mambo mazuri kwaajili yetu
na kututetea pale Shetani anaposhitaki. Damu inaisema kazi ya msalaba. Kwa njia
ya damu ya Yesu tunashinda mashitaka yote ya Shetani. Shetani hutumia dhambi
kuleta mashitaka hayo. Yesu alikufa kwaajili ya dhambi zetu, damu ya Yesu inao
huo ushuhuda. Shetani anapojaribu kutumia mashtaka kutuharibu au kutuchongea,
tunamshida kwa damu ya Yesu na neno la ushuhuda wa kazi ya Yesu kwaajili yetu
pale msalabani (Ufunuo 12:9-11). Kitu cha Muhimu tusiishi katika dhambi, kama tumetenda tutubu na kuendelea kushirikiana na Mungu
katika Agano, huku tukitamka kazi ya Yesu msalabani.
No comments:
Post a Comment