Saturday, August 16, 2014

Sehemu ya Kumi na Agano


Ibrahim na Mungu
Katika kitabu cha Mwanzo mlango wa 15 tunaona Mungu akifanya Agano na Ibrahimu kwa kumwambia ampatie wanyama kisha akapita katikati yao kwa mwenge wa moto. Alilithibitisha Agano yeye mwenyewe. Katika Agano Jipya Yesu alifanya Agano na wanadamu kwa njia ya kuutoa mwili wake na kumwaga damu yake na kila amwaminiye kama ni Myahudi au Mmataifa huiingia katika Agano.

Sura ya Kristo kwa Ibrahimu ilitokea kwa mfano wa kuhani Melkizedeki aliyeitwa kuhani wa Mungu aliye juu sana na mfalme wa Salemu(Mwanzo 14:17-20). Huyu alileta mkate na divai kwa Ibrahimu. Mkate  tunaweza kuufananisha na mwili wa Yesu katika Agano Jipya na divai ni damu yake. Melkizedeki amefananishwa na Kristo katika Agano Jipya (Waebrania 7:1,2, 10-22). Ibrahimu alimpa Melkizedeki sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. Katika Agano Jipya Yesu aliyekuja kwa mwili na damu yake kufanya Agano nasi, tunatoa sehemu ya kumi kwake, kama Ibrahimu alivyotoa kwa Melkizedeki. Kitendo cha kutoa sehemu ya kumi ni kitendo cha kiagano kwa yule aliyefanya Agano nasi yaani Yesu. Kwa hiyo kama Ibrahimu alikuwa baba yetu wa Imani naye alitoa sehemu ya kumi kwa Melkizedeki ambaye ni picha ya ‘Yesu Kristo’ katika Agano la kale, sisi pia tunaweza kutoa kwake Yesu leo, Sehemu ya kumi katika Agano Jipya.



No comments:

Post a Comment