Agano la Kale na
Jipya
Agano
la kale lilikuwa ni kivuli cha Agano Jipya lilianza wana wa Israeli walipotoka
Misri kama Taifa. Walitoka baada ya Damu ya
mwanakondoo wa pasaka kupakwa juu ya miimo ya milango yao. Agano hili liliisha Yesu Alipokufa
msalabani kama Mwanakondoo wa Mungu na kumwaga damu yake mwenyewe kama Mwanakondoo toka juu.
Imeandikwa,
“Angalia, siku zinakuja, asema BWANA,
nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. Si kwa mfano
wa agano nililoanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili
kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa
nilikuwa mume kwao asema BWANA. Bali agano hili ndilo nitakalolifanya na nyumba
ya Israeli, baada ya siku zile , asema BWANA; nitatia sheria yangu ndani yao,
na katika mioyo yao nitaiandika, nami nitakuwa Mungu wao nao watakuwa watu
wangu. Wala hawatamfundisha kila mtu na jirani yake, wakisema mjua BWANA;
kwamaana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa
miongoni mwao, asema BWANA; maana nitausamehe wala dhambi yao sitaikumbuka tena.” (Yeremia
31:31-33). Ni vizuri pia ukisoma maandiko yafuatayo, “Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami itatia roho mpya ndani yenu, nami
nitatoa moyo wa jiwe uliopo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.
Nami nitati aroho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi
mtazishika hukumu zangu na kuzitenda.” (Ezekieli 36:26-27).
Agano Jipya
Lililo Bora
Kwa
njia ya msalaba Yesu amekata Agano jipya lililobora. Sio kama lile la kwanza
lililosimama kwa damu za wanyama, hili limesimama kwa damu yake mwenyewe. Sio
kama lile la kwanza lililoandikwa katika gombo la chuo, na mbao za amri kumi,
bali hili limeandikwa mioyoni mwa waaminio kwa njia ya roho zao kuzaliwa mara
ya pili. Sio kama lile la kwanza, ambalo watu walikubaika kwa kujitahidi
kushika yote yaliyoandikwa katika torati, ingawa walishindwa. Sasa tunabarikiwa
kwa kuishi kwa amri ya upendo uliomiminwa na Roho Mtakatifu ndani yetu.
Upendo
hutuwezasha kushika amri zote, maana mioyo yetu imefanywa upya. Sasa hivi tuna
roho mpya au mioyo ya nyama iwezayo kushika amri za Mungu. Mungu alipoona watu
wake wameshindwa kushika sheria kwasababu ya roho zao kufa alifungua mlango wa
Agano jipya ambapo roho zitahuishwa hata kuweza kushirikiana nao na kuhusiana
nao kwa kuhifadhi na kushika ayatakayo.
Sasa
tunalo agano bora, Sio kama lile la kwanza ambalo watu walikubalika na Mungu
kwa kuitenda sheria. Agano hili ni la Neema watu wanakubalika na Mungu na
kuhesabiwa haki kwa kumwamini Yesu.
Katika
Agano la kwanza Shetani alikuwa na nafasi kubwa ya kutumikisha watu katika
dhambi maana asili zao zilikuwa ni roho zilizokufa. Katika Agano Jipya roho ya
mtu amwaminiye Yesu huwa huru chini ya sheria ya Roho wa uzima na kufungua
mlango wa kumshinda Shetani kwa uzima wa milele uliopo rohoni (Warumi 8:1-3).
Mtu
amwaminiye Yesu anakuwa si chini ya sheria ya dhambi na mauti, ambayo Shetani
aliitumia kutawala. Katika Agano la kwanza atendaye dhambi ilimpasa afe
kwaajili ya dhambi zake. Katika Agano jipya lililobora Yesu amekufa kwaajili ya
dhambi zote, wale wamwaminio wanatolewa katika adhabu ya dhambi zao, yaani
hukumu.
Mungu
huyu aliyetimiza ahadi alizosema katika Agano la kwanza, ambalo lilikuwa kivuli
kwa kuthibitishwa kwa damu za wanyama, je ataacha kuzitimiza ahadi zake katika
Agano hili lililothibitishwa kwa damu ya Mwana wake Yesu Kristo?
Agano
la kwanza la Mungu na Israeli lilikuwa na makuhani wanyonge waliozuiliwa na
mauti kuwa makuhani siku zote. Agano Jipya tuna Kuhani mkuu wa milele
asiyeweza kufa na aliye juu. Huyu ni kuhani halisi ambaye kivuli chake
kilionekana kwa kupitia makuhani wa Agano la Kale (Waebrania 7:28).
No comments:
Post a Comment