Waombee Unaowahudumia
Tarehe
31.1.2006, Roho wa Mungu aliniongoza moyo wangu kwa maneno haya “Waombee unaowahudumia, angalia mfano wa
Paulo”. Baada ya kupata ufahamu huu,
nikagundua ya kuwa mtume Paulo aliwaombea sana
watu aliowahudumia, pia alihitaji maombi kutoka kwao.
Baada
ya muda mfupi nilipata mawazo ya kufundisha somo ambalo litaonyesha ni jinsi
gani kanisa la kwanza waliomba na waliwaombea watumishi, pia jinsi gani
watumishi waliwaombea waumini. Kati ya
Maombi ambayo niliyaona katika maandiko, waliyoyaomba watumishi hawa, yalikuwa ni ‘maombi ya utimilifu’. Haya ni maombi yaliyoombwa kwaajili ya mtu
ambaye tayari amempa Yesu maisha yake.
Kwa
wakati wa sasa ni maombi ambayo
Mchungaji, Mwinjilisti, Mmishionari, Mwalimu, Shemasi au mtumishi mwingine
yoyote wa Mungu anaweza kuwaombea watu anaowahudumia. Kwa upande mwingine maombi haya yanaweza
kuombwa na watu wanaoipokea huduma hiyo, yaani kuwaombea wanaotoa huduma kwao.
Twaomba
Kutimilika Kwenu
Paulo
aliwaandikia Wakorintho, “Maana
twafurahi, iwapo sisi tu dhaifu, nanyi mmekuwa hodari. Tena twaomba hili nalo kutimilika kwenu”
(2 Wakorintho 13:9). Pamoja na kuuona uhodari wao kama yasemavyo maandiko haya, Paulo aliona hiyo bado haitoshi na hivyo kuongeza maombi ya utimilifu kwao. Mahali pengine aliandika, “Hatimaye ndugu kwaherini; mtimilike…” (2 Wakorintho 13:11). Maombi na matamshi ya mtumishi huyu wa Mungu kuhusu kutimilika aliyafanya kwa watu aliowahudumia.
(2 Wakorintho 13:9). Pamoja na kuuona uhodari wao kama yasemavyo maandiko haya, Paulo aliona hiyo bado haitoshi na hivyo kuongeza maombi ya utimilifu kwao. Mahali pengine aliandika, “Hatimaye ndugu kwaherini; mtimilike…” (2 Wakorintho 13:11). Maombi na matamshi ya mtumishi huyu wa Mungu kuhusu kutimilika aliyafanya kwa watu aliowahudumia.
Katika
kitabu cha Wakolosai 4:12, Paulo alimuelezea Epafra kama ifuatavyo, “Epafra , aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu
Kristo awasalimu akifanya bidii (bidii
hapa ni hali ya kumaanisha katika moyo, ni hali ya kuomba kwa mfano wa mtu
apiganaye mieleka) siku zote kwaajili
yenu katika maombi yake ili kwamba msimame wakamilifu
na kuthibitika (kusimama) katika
mapenzi yote ya Mungu”
Katika
maandiko haya yote Paulo alitumia neno Kutimilika
au Wakamilifu akiwa na maana ya;
(i) Kuwa kamili (ii) Kurejeshwa na (iii) Kukua katika tabia ya Kristo. Maahali pengine kuhusiana na kukua katika
tabia ya Kristo aliandika, “vitoto
vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu” (Wagalatia 4:19). Kwa maneno mengine katika maandiko haya Paulo
alikuwa anasema, “ Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu katika maombi
yangu kama mwanamke aliye karibu na kujifungua,
nafanya hivyo mpaka tabia ya Yesu iumbike ndani yenu, yaani izaliwe ndani yenu
ili mtimilike”
Maombi
waliyoomba Paulo na Epafra kuhusu utimilifu yalikuwa sawa na Yesu alivyosema
alisema, “Basi ninyi mtakuwa wakamilifu kama
Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”(Mathayo 5:48). Neno hili “Wakamilifu” limefanana na
“Watimilifu” katika lugha ya Kiyunani.
Ukamilifu aliousema Yesu hapa unahusiana na kufanana na Mungu kitabia, hasa wema wake, kama vile kuwatendea mema wote wabaya kwa wema.
Kama vile watumishi tuliowasoma kwenye maandiko walivyofanya
maombi ya kuombea utimilifu, sisi pia tunaweza kujiombea wenyewe na kuombea
wengine, hasa wale tunaowahudumia. Kuna
maeneo kadhaa ya ukamilifu/utimilifu ambayo tunaweza kuyaombea katika maisha ya
mtu, Tutayaangalia maeneo haya toleo linalofuata.
No comments:
Post a Comment