Kazi Njema
Pamoja
na kutaja baadhi ya kazi mbaya za ulimi, pia Kuna kazi njema. Mungu alipomuumba mtu alimuumba mkamilifu
asiye na shida baada ya anguko ulimi ulipata shida.
Kutenda Kazi
na Mungu
Mungu
ameweka ulimi katika viungo vya mwanadamu kama
chombo cha kumiliki na kutawala. Biblia
inasema “Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa
na ndege wa angani na kila mnyama wa mwituni”(Mwanzo 2 : 20). Msitari wa kumi na tisa unaonyesha kila jina alililoita
wanyama ndilo lilikuwa jina la wanyama hao.
Hii inaonyesha kwa sehemu Adamu alikuwa na mamlaka ya kusema kitu na kikawa. Mungu alimuumba Adamu na alimshirikisha
kutenda kazi pamoja na yeye. Mungu alimshirikisha kazi yake kwa njia ya kutoa
majina kwa ulimi . Sasa kwa njia ya Yesu
Kristo tunao uweza ule ule wa kumiliki
kwa njia ya Neno lake
tuliwekalo mioyoni mwetu. Kwa ulimi tutaweza kuwa watenda kazi na Mungu
kwa Neno lake. Mungu aliumba vitu vyote baadaye
akashirikiana na Adamu kuwapa majina kwa
ulimi wake. Sasa amemtoa Yesu na
anashirikiana nasi kutenda kazi yake ametupa huduma ya upatanisho kwa neno la
upatanisho katika vinywa vyetu (2 Wakorintho 5 : 19). Kwa njia ya ulimi
tunatenda kazi na Mungu kwa Neno kale, “Nao
wale wakatoka, wakahubiri kote kote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na
kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.” (Marko 16:20). Bwana
alilithibitisha Neno walilolihubiri mitume kupitia ndimi zao. Kwa ulimi waliunganishwa na ulimwengu wa
miujiza kwa Neno la Mungu. Hilo linatokea hata kwetu,
tunapojaza neno mioyoni na kulisema kwa ufunuo wa Roho. Mungu huanza kutenda
kazi na sisi hii ni kazi njema ya ulimi.
Pia
kwa njia ya maombi mapenzi ya Mungu hutimia duniani kama
mbinguni, kwa njia ya ulimi maombi haya hutendeka. Ulimi mmoja unaweza
kubadilisha ukoo, nchi na hata dunia kwa
njia ya maombi. Mungu anapotaka kutenda
mapenzi yake duniani huliweka neno lake
kinywani mwa mtu.
Kutakaswa
Kwa
njia ya ulimi tunatubu na kutakaswa dhambi zetu. Kwa njia ya ulimi uhusiano wetu na Mungu
unarejeshwa kwa toba na utakaso wa dhambi kupitia damu ya Yesu. Unaweza kusoma (1Yohana 1:9). Katika kitabu
cha Warumi imeandikwa, “Wala msiendelee
kuvitoa viungo vyenu kuwa silaha za
dhuluma kwa dhambi, bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama walio hai baada ya
kufa, na viungo vyenu kwa Mungu kuwa silaha za haki,”(Warumi 6 :13). Msitari wa kumi na tisa unasema “…kwa kuwa kama
mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo
sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa.” Ndimi zetu
zinapotumiwa na haki huleta utakaso katika maisha. Hii hutokea ndimi zetu zinapokuwa chombo cha
Neno la Mungu maana Neno hutakasa. Tuliona mwanzoni yatokayo moyoni humtia mtu
unajisi. Lakini pia yatokayo moyoni,
moyo ulio na Neno la Mungu hutakasa, ulimi unatia unajisi ikiwa moyo hauna
Neno, lakini pia unayo kazi ya kutakasa kwa Neno.
Kutukuza
Biblia
haituonyeshi moja kwa moja kama Adamu aliutumia
ulimi wake kumtukuza Mungu. Mimi ninaamini alipoumbwa aliishangaa uumbaji ambao
Mungu aliufanya kabla hajamuumba.
Inawezekana kabisa baada ya kuushangaa alimwinua na kumtukuza kwa ulimi
wake. Tutangalia sehemu mbili katika
maandiko ambazo zinaonyesha kazi ya ulimi ni kumtukuza Mungu. Unaposoma maandiko haya angalia sehemu
nilizokoleza na uzifananishe utajifunza vizuri zaidi. “Nimemweka BWANA mbele yangu daima, kwa kuwa yuko kuumeni kwangu, sitaondoshwa. Kwa hiyo moyo wangu unafurahi nao utukufu wangu unashangilia….”(Zaburi 16:8-9). “….Nalimwona Bwana mbele yangu sikuzote, kwa
kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume nisitikisike. Kwa hiyo moyo wangu ukapendezwa Ulimi wangu ukafurahi;” (Matendo 2
: 25-26) kwa maandiko haya mawili tunaweza kusema ulimi wa mtu ni utukufu
wake. Ulimi wa mtu ni chombo cha utukufu
wa Mungu. Hii ilionekana wakati wa siku
ya Pentekoste walipojazwa Roho Mtakatifu walisikiwa wakitumia ndimi zao
kumtukuza Mungu. “Wakrete na Waarabu;
tunawasikwa hawa wakisema kwa lugha zetu
matendo makuu ya Mungu” (Matendo ya Mitume 2 : 11). Ndimi zetu zimeumbiwa utukufu wa Mungu. Shetani anataka sana kuharibu jinsi, tunavyoongea kwa kuwa
mara zote hupenda kutumia visivyo (mis-use) vitu vya Mungu. Neno lolote ambalo halimpi Mungu utukufu,
litokapo katika vinywa vyetu, hutufanya kuutumia ulimi pasipo makusudi yake.
Katika kitabu cha Wakolosia imeandikwa “Na
kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu,
mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”(Wakolosai 3:17). Maneno tusemayo ambayo yanaleta msukumo kwa
tuyatendayo inapasa yawe kwa utukufu wa Mungu.
Maneno inapasa yaonyeshe kumwinua na kumtukuza Mungu hiki ni moja ya
kipimo cha maneno yetu. Je yanampendeza Mungu? Kama
yanampendeza basi yanamtukuza. Kazi ya
ulimi ni kumtukuza.
Kukiri
Yesu
ni kichwa cha Kanisa ni kuhani wetu mkuu mbele za Mungu. Amekwenda mbinguni
kwaajili yetu, yupo mkono wa kuume wa Mungu kwaajili yetu. Je, tunaunganishwa naye kwa jinsi gani? Ni kwa
maungano yetu. Biblia inasema, “ Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki
mwito wa mbinguni, mtafakarini sana
mtume na kuhani mkuu wa maungano yetu, Yesu,”(Waebrania
3 : 1).
Jinsi
tunavyoongea duniani kama vile neno lisemavyo
tuna ‘m-keep bize’ Yesu mbinguni. Tunampa
matirio yaani maneno ya kuyafanyia kazi kama kuhani. Kukiri ni kusema kama
Mungu asemavyo katika maandiko.
Tunasema
kama Neno lisemavyo, tunasema Yesu alitufanyia nini msalabani, alipofufuka na
alipoketi mkono wa kuume. Tunasema sisi
ni nani kwake, yeye ni nani kwetu, tunasema kama
Neno lisamavyo. Imani ya Neno la Mungu
huanzia mioyoni mwetu na utimilika vinywani mwetu. Imani hii iwapo kinywani kwa
njia ya maneno tusemayo humwingiza Yesu kazini. Yesu amepewa mamlaka yote
mbinguni na duniani. Anapata nafasi
duniani kwa maneno yetu yaliyosawa na Neno lake. Tunapotamka maneno haya, mamlaka ya utendaji
wake hujidhihirisha. Biblia inasema, “Basi
iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia
katika mbingu, Yesu mwana wa Mungu na tuyashike sana maungano yetu,” (Waebrania 4 :14).
Tunayashika maungano yetu, yaani maneno yetu yalisemalo Neno lake maana
ameingia katika mbingu kwaajili yetu, ayahudumie maungano yetu.
Wakati fulani nilipompa Yesu maisha yangu mwezi wa
kumi mwaka 1989 moyoni mwangu nilipata ushuhuda usemao “Amini usemayo”. Yalikuwa ni
maneno yaliyojirudiarudia ndani yangu. Siku moja nilikutana andiko linalofana
na mawazo hayo linasema, “Lakini kwa kuwa tuna roho ile ile ya imani kama ilivyoandikwa, naliamini na kwasababu hiyo nalinena; sisi
nasi twaamini na kwasababu hiyo twanena”(2Wakorintho
4:13). Imani iliyopo moyoni husema
kinywani. Kile unachokijua kuhusu Mungu,
kuhusu wewe katika Mungu au ushindi wako katika Kristo utakisema kwa kinywa
chako, pia utakitarajia kudhihirika kwa kuwa unaye kuhani aliyesimama mbinguni
kwaajili yako, ili adhihirishe maungano au maneno yako ya imani.
No comments:
Post a Comment