Monday, August 25, 2014

Imani Inatenda kwa Upendo


Ifahamu Imani na Upendo
Ili kuweza kuishi kwa imani itendayo kazi ni lazima ufahamu ya kuwa imani yako hufanya kazi pamoja na upendo.  Kama vile samaki asivyoweza kuishi akitolewa nje ya maji, imani haiwezi kuishi au kutoa matunda yadumuyo isipokuwa ndani ya upendo.  Msingi wa imani ya kweli mbele za Mungu ni upendo.  Maandiko yanasema, “Maana katika Kristo Yesu kutairiwa hakufai neno, wala kutotahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo” (Wagalatia 5:6).

Kuishi kwa Upendo ni nini?

Kwa kuwa tumefahamu kwamba imani inatenda kazi kwa msingi wa upendo, ni muhimu tuelewe tunaishije kwa upendo.  

Kuzishika/ Kuzitii Amri za Mungu

Maandiko yanasema, “Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu” (1 Wakorintho 7:19).  Kuzihifadhi amri au kuzishika amri ni kumpenda Mungu, ni kuishi kwa upendo mbele za Mungu.  Yesu alisema, “Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye;…” (Yohana 14:21).  Mtumishi wa Mungu Yohana kwa Roho Mtakatifu aliandika, “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.” (1Yohana 5:3).  Maandiko haya yote yanaonyesha ya kuwa kumpenda Mungu ni kuzishika amri zake.  Unazishika amri zake ingawa hatumuoni.  Ndani yetu una uhakika yeye ni dhahiri ni bayana ndio maana tuna mtii.
Tunapoishi kwa kumtii Mungu, yaani tunapoishi kwa kulitii Neno lake ni udhihirisho kuwa tunampenda.  Ikiwa unampenda mtu si rahisi kuacha kufanya anachokuambia. Tumpendapo Mungu tutafanya ayatakayo.  Ingawa hatumwoni kwa macho, mioyo yetu inamwona dhahiri yupo kwa njia ya Neno lake. Katika hali ya kumpenda ni rahisi kuwa na ujasiri mbele zake maana dhamiri zetu hazita tushitaki kwa kosa lolote.[1]  Ujasiri huu utatuwezesha kuomba kwa imani na kupokea.  Kwa maneno mengine imani yako katika maombi itafanya kazi kwa kuwa umempenda Mungu kwa kumtii hata kuwa na ujasiri mbele zake.  Maandiko yanasema, “ na lolote tuombalo (Tuombalo kwa imani), twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake(twampenda twaenenda kwa upendo), na kuyatenda yapendezayo machoni pake.” (1 Yohana 3:22). 

1.     Kuishi kwa Mwongozo wa Roho Mtakatifu/ Kuishi kama Viumbe Vipya

Tunapookoka/tunapompa Yesu maisha yetu tunafanyika viumbe vipya.  Katika utu wa ndani tunakuwa tumezaliwa na Mungu, hivyo tunafanana na Mungu aliye Upendo.  Kila mtu aliyempokea Yesu/ aliyezaliwa mara ya pili, anao upendo wa Mungu ndani yake (Warumi 5:5).  Inawezekana hautumii au haishi kwa kuongozwa na upendo, lakini tayari umepandwa ndani kwa njia ya Roho Mtakatifu.  Maandiko yanasema, “Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya (au kuzaliwa mara ya pili)” (Wagalatia 6:15).  Kuzaliwa mara ya pili kumefanyika kwa njia ya Mungu Roho Mtakatifu ndani yetu, “Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho” (Yohana 3:6).  Ikiwa mtu amezaliwa kwa Roho Mtakatifu kwa njia ya kumwamini Yesu, katika upya huo wa kiroho, Roho wa Mungu huanza kumuongoza mtu huyo kwa njia ya tunda la Roho, yaani upendo.  Roho  Mtakatifu anamsaidia mtu huyo kupenda, kupenda ni; kusamehe, kuvumilia, kufadhili, kutohesabu mabaya, kuwa na amani, kuwa na furaha, nk.  Maisha ya namna hii ni maisha  ya upendo yaiwezeshayo imani ya mtu aliyeokoka kufanya kazi.

Maneno Aliyosema Yesu


 Mifano ya utendaji wa imani pamoja na upendo tunaweza kuipata katika mafundisho aliyofundisha Yesu.   Alisema, “Nanyi msimamapo na kusali (kusali ni tendo la imani), sameheni (kusamehe ni tendo la upendo), mkiwa na neno juu ya mtu;…”(Mathayo 11:25).  Mahali pengine alisema, “Basi ukileta sadaka yako (kitendo cha kutoa/kuleta sadaka ni kitendo cha imani) madhabahuni na huku ukikumbuka ndugu yako ana neno juu yako, iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako(kupatana na ndugu ni upendo), kisha urudi uitoe sadaka yako.” (Mathayo 5:24-25).  Kwa maandiko haya tunagundua kuwa huwezi kuchukuwa hatua ya imani ya kuomba au kutoa, ikiwa una tatizo katika upendo, yaani haujasamehe au haujamtii Mungu. Upendo ndani yako unajenga uhalisi na ujasiri wa kupokea mambo unayoarajia.
Ili kuchochea utendaji wa imani yako ni lazima utafute sana kuishi kwa upendo mbele za Mungu na watu.  Ukiishi kwa upendo utafahamu kuwa Mungu yuko upande wako na anaiheshimu imani yako.  Utakuwa na ujasiri mbele zake kwa kuwa hauna hatia kwake, umemtii, unampenda.   Ufahamu huu utaichochea imani, uhalisi wa ndani, kutegemea muujiza toka kwa Mungu wako.
Chochea imani yako kwa njia ya kumtii Mungu na maneno yake yote, na kuwa na amani na watu wote.  Kisha utakuwa na ujasiri wa kupokea kwa imani toka kwa Mung

 





No comments:

Post a Comment