Fahamu
ya Kuwa Mungu Habadiliki
Ni
vizuri kumfahamu Mungu huwa ana tabia gani katika utendaji wake, ili
upokee mahitaji yako.
Mungu
Habadiliki
Mungu
uliyenaye ni Mungu asiyebadilika, ni Mungu asiye na kigeugeu.
Maandiko yanasema, “Mungu
si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute (abadilishe
nia au mawazo yake);
(Hesabu
23:19). Mungu hageuki geuki na kubadilika kama watu wafanyavyo.
Andiko lingine linasema, “Kwa
kuwa mimi, BWANA,
sina kigeugeu;
ndio maana ninyi hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo.
(Malaki 3:6). Mungu ni Mungu wa maagano na watu wake, hageuki na
kuacha ahadi au Agano lake na watu wake. Ndio maana mahali pengine
Mungu anasema, “Mimi
sitalihalifu (sitalivunja)
agano
langu, Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu”
(Zaburi 89:34). Maandiko haya yote yanaonyesha ya kuwa Mungu
habadiliki.
Yesu
Habadiliki
Kuhusu
Yesu Biblia inasema, “Maana
Mwana wa Mungu, Kristo Yesu, aliyehubiriwa katikati yenu na
sisi…hakuwa Ndiyo na siyo; bali katika yeye ni Ndiyo.”
(2 Wakorintho 1:19). Andiko hili linaonyesha kuwa Yesu habadiliki,
na kuwa ndiyo na siyo, yeye sikuzote ni NDIYO. Andiko lingine
linaloonyesha ukweli huu linasema, “Yesu
Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.”
(Waebrania 13:8).
Kama
Alivyotenda Ndivyo Atendavyo
Kwa
maandiko haya inakupasa kufahamu kuwa Mungu/Yesu habadiliki. Kama
aliponya bado anaponya, kama alisamehe bado anasamehe, kama aliwapa
watoto wasiokuwa na watoto bado anafanya hivyo. Watoto wako wapo
kwake nawe unawapokea. Katika tatizo lako au hitaji lako ni vizuri
kumfikiria Mungu vizuri. Tafuta katika maandiko aliwafanyia nini au
aliwaambia nini watu waliokuwa na matatizo. Kisha ukumbuke kuwa
Mungu aliyewafanyia wengine mambo mema anaweza kukufanyia na wewe.
Kama vile Mungu alivyowaambia wana wa Israeli kuwa yeye ni Mungu
awaponyaye (Kutoka 15:26), hajabadilika ndiye akuponyae wewe LEO.
Kama vile Yesu alivyozunguka huko na huko na kuponya wagonjwa, yupo
sasa karibu nawe akuponye hajabadilika. Uponyaji upo karibu na wewe.
Muujiza wako upo karibu nawe maana unaye Mungu yule yule atendaye
miujiza siku zote. Tarajia kuwa ameyasikia maombi yako, kama
alivyowasikia watumishi wake mbalimbali katika Biblia ndivyo
akusikiavyo sasa. Tegemea kupokea Muujiza kwa Mungu wa miujiza
asiyebadilika, aliye dhahiri ndani yako kwa Neno lake, ingawa
haonekani.
Usomapo
Neno la Mungu ukumbuke ya kuwa Mungu hajabadilika, bado anatenda.
Usikate tamaa bado inawezekana!. Soma vitabu vya Injili uone Yesu
aliwafanyia nini wenye shida, Yote aliyofanya anakufanyia na wewe.
Kwa kuwa hajabadilika na hana upendeleo.
No comments:
Post a Comment