Fahamu
Uweza wa Jina la Yesu
Yesu
Kristo yupo juu ya kila kitu. Hawezi kuzuiliwa na kitu chochote
akiamua kutenda jambo. Anayo mamlaka yote na nguvu, alisema,
“…Nimepewa
mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni,
mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi,…”(Mathayo
28:18-19). Yesu anao uamuzi na uwezo wote wa kutenda mbinguni na
duniani. Kwa mamlaka hiyo amewaagiza watu wake waende ulimwenguni
kufanya kazi yake kwa nguvu na mamlaka yake.
- Unayo Mamlaka
Yesu
amekupa amri na mamlaka ya kwenda ulimwenguni. Mamlaka na nguvu zake
zipo katika jina lake. Ulitumiapo jina la Yesu ni kama vile
unamuachilia Yesu atende kazi katika mazingira yako. Jina la Yesu na
Yesu ni umoja. Yesu alisema, “…Enendeni
ulimwenguni mwote…Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa
jina langu watatoa pepo;…”
(Marko 16:15,17). Yesu aliposema enendeni,
aliambatanisha
neno hilo na mamlaka yake. Hatuenendi duniani kumtumikia kwa nguvu
zetu bali kwa mamlaka na nguvu zake. Je mamlaka hiyo na nguvu viko
wapi? Viko ndani ya jina lake. Hivyo unapotumia jina la Yesu
unaingia katika umiliki pamoja na Kristo Yesu.
Umepewa
Jina Kuu
Jina
hili lenye nguvu na mamlaka ni zawadi kwa Kanisa. Kwa Jina hili
Kanisa linatumia nafasi ya utendaji ya Yesu duniani kwa kuzifanya
kazi zake. Yesu amehamishia mamlaka yake na nguvu ndani ya Kanisa
kwa njia ya kulipa Kanisa Jina lake. Twaweza kusema Jina la Yesu
ndani ya Kanisa, yaani wale waliomwamini, ni Yesu mwenyewe atendaye
kazi kupitia wao, akiwa na mamlaka yake yote na nguvu kwa Roho
wake
Mtakatifu. Mungu hufanya kazi kupitia Kanisa katika ushirika
wa Roho Mtakatifu kwa Jina la Yesu.
Hivyo
usiogope chochote, amini kuwa utamkapo jina la Yesu Mungu atakusaidia
kwa mkono wake kukutetea katika mazingira yako ikiwa ni ugonjwa au
tatizo lolote.
Utamkapo
jina hili kuu, fahamu ya kuwa si wewe utendaye bali unamruhusu Yesu
atende katika mazingira yako kwa mamlaka yake yote na nguvu.
Kuazia
leo fahamu ya kuwa imani yako uliyoiweka katika jina la Yesu umeiweka
kwa Yesu mwenyewe. Utamkapo jina hili kwa ujasiri Mungu atafanya
kazi pamoja na wewe akimtukuza Yesu.
No comments:
Post a Comment