Friday, July 11, 2014

Ameifuta Hati



Exaleipho

Akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa kwa kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani”
(Wakolosai 2:14)

Neno kuifuta hapa tafsiri yake ni kuifuta kabisa pasibaki na alama yeyote kwamba palikuwa na maandishi.

Sheria ya Musa ilikuwa ni hati halali ya Ki-sheria iliyotushitaki kwamba sisi ni watenda dhambi na tunastaili mauti.

Kwa hali ya kawaida hatungeweza kutoka katika mashitaka hayo ya Sheria maana tulikuwa chini ya mwili wenye tamaa ya dhambi. Sheria ikawa na nguvu ya kutushitaki dhambi kwa kuwa dhambi ilikuwa hai kwa mwili (Warumi 8:3).

Msalabani Yesu alifanya vitu viwili:
1.)Alifuta mashitaka ya Sheria kwa kifo chake. Alilipia Sheria mauti,
maana ilitaka dhambi zilipiwe mauti. Sasa Sheria imefutwa mashitaka yake ya kutaka tufe, kwa kuwa kifo cha Yesu kimelipia matakwa hayo (Warumi 7:1-5).
2.)Amesulubisha mwili wa dhambi uliyoipa dhambi nguvu ya kufanya kazi ndani ya mtu. Dhambi iliyokaa mwilini ilimfanya mtu awe adui wa Mungu, maana sheria ilikuwa inaionyesha wakati wote.  Aliposulubiwa alisulubisha mwili uliotunza dhambi. Kwa njia ya mwili akafungua njia ya sisi kwenda kwa Mungu. Kwa njia ya damu akatupatanisha na Mungu (Waefeso2:15-16, Wakolosai 1:20).

Wazo  Kuu
Hati ya mashitaka juu yetu iliyotushitaki tufe imefutwa. Imefutwa kwa kifo cha Yesu. Nguvu yake imeondolewa kwa kuwa ameusulubisha mwili wa dhambi. Mwili huu uliipa Sheria nguvu ya kuukumu tufe kwa dhambi iliyokuwa ndani yake. Sasa, Shetani hana pa kutushikia maana alitupata kwa dhambi. Hatatumia sheria kudai tufe kwa mauti, hatatumia mwili kuchochea tamaa ya dhambi.
SOMA TENA, OMBA  NA KUTAMKA MANENO HAYA KABLA YA KUANZA KAZI ASUBUHI, PIA KABLA YA KULALA TAFAKARI, AU SHIRIKISHANENI KATIKA KIKUNDI NA IBADA YA NYUMBANI.










No comments:

Post a Comment