Saturday, July 12, 2014

Shetani Amefedheheshwa Mshangilie Yesu



Deigmatizo

“Akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia kwa msalaba huo.”
(Wakolosai 2:15)

Yesu msalabani alipomnyang’anya Shetani mamlaka na kumfanya si kitu alimfedhehi kwa dhahiri. Alionyesha fedhea ya kushindwa kwake waziwazi. Neno “Deigmatizo” kwa Kiyunani ni kufedhehesha. Katika Mathayo 1:19, limetumika kwa maana ya, kuaibisha. Yusufu alikuwa hataki kumwaibisha Mariamu.

Shetani, Wayahudi na Warumi walimwaibisha Yesu msalabani kwa kumvua nguo, kumtemea mate, kumdhihaki nk.

Kitu cha ajabu msalaba huo huo ukageuka kuwa silaha ya kumwaibisha Shetani hadharani kwa dhahiri.

Wafalme wa zamani waliposhinda vita, mfalme aliyeshindwa alifedheheshwa kwa kupitishwa barabarani, kuzomewa, kutupiwa vinyesi, wakati huo huo aliyeshinda alikuwa akishangiliwa.

Hivi ndivyo ilivyotokea, Yesu alipokufa na kufufuka; Amemnyanganya Shetani silaha zote, ikiwepo silaha kuu iitwayo mauti! (Ufunuo 1:18). Amefufuka kwa kushinda, tumshangilie kwa sifa na hapo hapo tutangaze kushindwa kwa Shetani.Twaweza kufanya hivi katika maombi, sifa au uinjilisti.
  
WAZO KUU
SIFA, MAOMBI, NA UINJILISTI UAMBATANE NA KUTANGAZA KUSHINDA KWA YESU NA KUSHINDWA KWA SHETANI. HII ITADHIHIRISHA UKWELI HUO KATIKA MAISHA YETU.

No comments:

Post a Comment