Friday, June 27, 2014

Usitupe Ujasiri



Usiutupe Hata Akinguruma
Tunahitaji ujasiri katika imani zetu ili tupokee jambo, au tuweze kushindana.
Basi msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu........”
(Waebrania 10:35)
Msitari wa 32 na 33, kabla mwandishi hajawaandikia Waebrania  wasiutupe ujasiri, aliandika kwamba wazikumbuke siku za kwanza baada ya kutiwa nuru walishindana mashindano makubwa. Waliweza kustahimili mambo magumu na hapohapo kutenda mema. Bila shaka kitu kilicho wawezesha kuwa hivyo ni ujasiri ndiyo maana msitari huu wa thelathini na tano akaandika wasiutupe ujasiri maana uliwasaidia kwanza.
Apobalo
Kutupa ujasiri ktika andiko hili, ni sawa na kutupa silaha huku ukiogopa! Neno “Apobalo” la Kiyunani, lilitumika kuonyesha askari anayetupa silaha huku akiogopa baada ya kumwona adui. Kwa lugha nyingine adui huyu alikuwa anafanya vitu vya kumwogopesha ili autupe ujasiri. Roho ya woga iletwapo na Shetani shabaha yake ni tutupe ujasiri na kuimbia. Pasipo ujasiri hatuwezi kusimama na kutumia silaha yeyote!
MAMBO MUHIMU YA KUYAFAHAMU
1.   Shetani Hushambulia Ujasiri (1Petro 5:8)
-      Hutishia kwa kutumia vitu unavyoviona mfano: ukibanwa na kifua au ukiishiwa pesa. Hali hizi zinaweza kutumika kukufanya uutupe ujasiri katika Bwana. Ukitupa ujasiri huwezi kushindania ushindi wa Yesu.
-      Adui ataweza nguruma kwa hali hizi, kukuonyesha katika mawazo, ukimwachia aendelee bila kutamka Neno utatupa ujasiri na atakupata.
-      Hauutupi ujasiri kwa kumpinga ukiwa thabiti katika imani ya Neno kinywani mwako.

Mfano wa Daudi  Hakutupa Ujasiri Akatumia Silaha (1Samweli 17:4 – 11)
1.   Shetani alinguruma kupitia mazingira (Goliati)
2.   Israeli wakatupa ujasiri wao na kukimbia (17:24)
3.   Daudi hakutupa ujasiri kwasababu hiyo akaweza kumkabili (1Samweli 17:37,17:45 – 48). Aliweza kutotupa ujasiri kwa imani yake katika Bwana.
Mfano wa Petro  Alitupa Ujasiri Akaanza Kuzama (Mathayo 14:22 – 30)
1.   Alisikia Neno la Yesu “Njoo”
2.   Shetani akanguruma kwa kumwonyesha upepo
3.   Alipoangalia upepo akatupa ujasiri, akaanza kuzama
4.   Angeweza kutotupa ujasiri kwa kuzidi kumtazama Yesu aliyemwita “Njoo”
Wana wa Israeli  Walitupa ujasiri Hawakuingia Kanani (Hesabu 13:27 – 30,23 – 25)
1.   Waliona majitu
2.   Wakajitazama wao walivyo, badala ya kumtazama Mungu aliye pamoja nao.
3.   Walipotazama majitu yalivyo, Shetani akanguruma wakatupa ujasiri
4.   Wangemtazama Mungu kama Daudi wasingetupa ujasiri
FAIDA ZA UJASIRI
1.   Kuweza kupokea ahadi kinyume na mazingira magumu yanayoonekana.
2.   Kuweza kusimama mbele za Shetani na kumshinda kwa kutumia silaha za kiroho
3.   Kuzalisha matokeo katika mazingira tatanishi,
                  Ujasiri una thawabu, Una matokeo Usiutupe

2 comments:

  1. BLESSED BE THE NAME OF THE LORD GOD, I REALLY NEEDED THIS LESSON. BLESS YOU PASTOR.

    ReplyDelete
  2. Amen. Asante Naomi kwa Kusaidika kwa Ujumbe huu.

    ReplyDelete