Hatua za Kupokea Toka
kwa Mungu
“Kwa
sababu hiyo nawaambia , Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu”
(Marko 11:24)
Kupokea katika andiko hili
kumegawanyika sehemu mbili:
1. Amini Unapokea
Uombapo saa hiyo hiyo unapokea katika ulimwengu wa roho,
ulimwengu war oho hauna muda kila kitu ni sasa unapokea sasa, ila ulichopokea hakionekani katika ulimwengu wa mwili,
ulimwengu wa mwili una muda.
2. Nayo Yatakuwa Yako
Ulichopokea sasa, hakionekani katika muda huu, lakini kipo ni
chako rohoni kwa Neno la Mungu, unacho! Yatakuwa
yako maana yake yatadhihirika. Ulichopokea tayari ROHONI kitadhihirika
KATIKA MUDA WA MWILINI, ila unacho tayari.
ZIFAHAMU HATUA HIZI
1. Lifahamu Neno Husika: Neno la Mungu ndilo linatupa mahitaji yetu. Kama ni ugonjwa
linauponyaji wetu (1Petro 2:24). Kama ni laana lina Baraka zetu (Wagalatia
3:13). Kama ni kutoweza neno ni kuweza kwetu (Yohana 15:5, Wafilipi 4:13). Chochote unachohitaji tafuta Neno husika
lililonacho hata kama ukioni. Uwe na
“note book” na andika hatua ya kwanza HITAJI NA NENO LAKE.
2.Yashike Yatarajiwayo
kwa Hilo: Unachotaka
kidhihirike kipokee sasa toka kwenye hilo Neno kwa kukiomba. Sema kwa mfano,
“Baba kwa jina la Yesu naomba nitie nguvu nimalize mtihani maana imeandikwa
nayaweza yote katika yeye anitiaye nguvu (Wafilipi 4:13). Baba unanitia nguvu
kwa Neno hili sasa. Nayo yanakuwa yangu nauona udhihirisho natiwa nguvu”.
3.Usifungwe na
Mazingira: Baada ya
kuomba hivi unaweza kuona udhaifu ndio unazidi! Usemeshe, mara nyingine uamuru
uondoke na kuamuru Neno uliloomba ambalo umesha lipokea litokee kwa jina la
Yesu. Kipengele hiki ni cha vita ya imani. Ambayo hupiganwa kinyume na
mazingira yanavyoonyesha. Yesu aliongea na upepo, mazingira yakabadilika
(Mathayo 8:26).
4.Tenda Jambo: Kuamini maana yake ni kutenda Jambo fulani
nje kutokana na jibu ulilokwishapokea kiroho. Kutenda imani ni pamoja na
KUSHUKURU ulilopokea moyoni kabla hujaona mwilini katika muda. Kuamini pia ni
KUSEMA yasiyooneka, ambayo tayari umeyapokea kana kwamba yameonekana
(2Wakorintho 4:13).
5.Ishi kwa Upendo: Imani inazaa matunda na kutenda kazi
ndani ya upendo (Wagalatia 5:6). Imani
inaishi kwa upendo. Upendo ni kutenda kama Mungu asemavyo (Yohana
14:21,23). Upendo ni kumfanyia kitu mtu
ambacho ungependa ufanyiwe (Mathayo 7:12). Upendo ni kuongozwa na Roho
Mtakatifu kitabia (Wagalatia 5:22). Utendapo tendo la imani, kwa mfano kuomba
lazima uwe na upendo yaani kusamehe (Marko 11:25). Kama unatenda tendo la imani
la kutoa sadaka lazima liambatae na upendo wa kusamehe ili lizae. Wakati utendapo
tendo lolote la imani, lazima mahusiano yako na Mungu na watu yawe ya upendo.
SOMA HATUA HIZI NA KUZIRUDIA, KISHA
ZITUMIE KATIKA MAHITAJI YAKO, UTAONA MAJIBU
No comments:
Post a Comment