Ukiri
wa Imani
Katika
agano jipya kuna mambo Yesu alikuja kuyafanya kwaajili yetu, ambayo tukiykiri
kwa imani tutakuwa tunaachilia nyugu ya Agano. Kila nikiamka asubuhi au kabla
ya kulala huyakiri haya naamini nitafanya hivyo maisha yote. Karibu na wewe
kukiri haya ili tuliishi Agano kwa imani. Mambo haya Roho Mtakatifu
alinifundisha tarehe 19.9.2010 nilipokuwa na hudumu maeneo ya Sagara Singida.
Mwili na damu ya Yesu ndio chanzo cha Agano jipya. Kabla hujashiriki meza ya
Bwana unaweza kuyakiri mambo haya na yatathibitika kwako kama
Agano. Utakuwa ukifanya ukumbusho wa kazi ya Yesu aliyoifanya msalabani kwa
mwili na damu kwaajili yako.
Sema
Yesu Alimfanya Nini Shetani Kwaajili Yako
- Alimharibu kwa mwili wake kwaajili yako (Waebrania 2:14). Sema hivyo.
- Aliziharibu kazi zake zote kwaajili yako (1Yohana 3:8). Sema kama neno lisemavyo.
- Alimfanya si Kitu akamnyanganya silaha kwaajili yako (Wakolosai 2:15). Patana na andiko hili na kulisema.
- Yesu alituokoa toka katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake. Sema Yesu ameniokoa toka nguvu za giza nipo ndani ya ufalme mwingine, ufalme wa Mungu (Wakolosai 1:13-14).
- Alimfadhaisha Shetani hadharani (Wakolosai 2:15). Sema haya, aliyafanya kwaajili yako. Unaweza kuongezea maandiko mengine.
Sema
Yesu Alifanya nini mbele za Mungu kwaajili yako
- Aliingia mbele za Mungu kwaajili yako, sema unaweza kuingia hapo kwa ujasiri (Waebrania 9:24). Sema kama neno lisemavyo.
- Aliharibu mashitaka ya Torati iliyokuwa inanishitaki mbele ya haki ya Mungu. Aliharibu kwa njia ya kuyasulubisha mashitaka yake kwa yeye kufanyika dhambi na kusulubiwa (Wakolosai 2:14). Tamka kwamba imetokea kwako, torati haina nguvu kwako.
- Sema Yesu alifanya amani mbele za Mungu kwa damu ya msalaba wake. Ninaweza kumkaribia Baba bila woga kwa damu ya Yesu (Wakolosai 1:20).
Sema Wewe ni nani katika Yesu
- Sema “Mimi ni mjumbe ni balozi wa Mungu”. Sema “Nipo duniani kusema kwaajili ya mbinguni” (2Wakorintho 5:20).
- Sema “Nimezaliwa kwa mbegu ya mbiguni neno la Mungu ninafanana na Neno lake” (1Petro 1:23).
- Sema “Nimenunuliwa kwa damu ya thamani, hiyo inaonyesha uthamani wangu, sijanunuliwa kwa fedha bali kwa maisha ya Mungu, yaani damu yake” (1Petro 1:18-19).
- Sema “Wenyeji wangu ni mbinguni sio duniani. Ninazo hali za mbinguni si za duniani” (1Petro 2:9). Unaweza kuongezea maandiko.
Sema Una kitu gani ndani ya
Yesu
- Sema ninayo Amri ya kukanyaga nyoka na nge na nguvu zote za giza (Luka 10:19).
- Ninalo tumaini la uzima wa milele kwa njia ya Yesu kufufuka katika wafu (1Petro 1:3).
- Sema ninao uzima wa milele, nguvu ambayo inamfanya Mungu awe Mungu (Yohana 3:16).
- Sema Bwana ni mchungaji wako hautapungukiwa unayo unayohitaji (Zaburi 23:1-2).
- Unaye Mungu aliye upande wako hakuna aliye juu yako, sema hivyo (Warumi 8:31).
- Sema aliye ndani yako ni mkuu kuliko aliye katika ulimwengu. Roho wa Mungu, Yesu Kristo, Mungu Baba ndani yangu ni mkuu. Mkuu kuliko uchawi, pepo na uharibifu wote (1Yohana 4:4).
Mfumo wa ukiri katika maisha
yako unaweza kuuanza kupitia mambo haya manne. Ukianza kukiri Mungu atazidi kukupa
ufunuo na imani yako itaongezeka. Ongezea maandiko hayatoshi haya niliyoyataja.
Kiri kila unapoamka au kabla ya kulala. Unaposoma Biblia hasa Nyaraka za Mitume
ongeza maandiko. Baada ya muda kupita utaongeza imani yako na kushinda kwa
ukiri wa imani.
Kuhani wa Maungamo
Yesu
ni kichwa cha Kanisa ni kuhani wetu mkuu
mbele za Mungu. Amekwenda mbinguni kwaajili yetu, yupo mkono wa kuume wa Mungu
kwaajili yetu. Je, tunaunganishwa naye
kwa jinsi gani? Ni kwa ukiri wetu.
Biblia inasema, “ Kwa hiyo, ndugu
watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana mtume na kuhani mkuu wa maungano yetu,
Yesu,”(Waebrania 3 : 1).
Jinsi
tunavyoongea duniani kama vile neno lisemavyo
tuna ‘m-keep bize’ Yesu mbinguni.
Tunampa malighafi, yaani maneno ya
kuyafanyia kazi kama kuhani. Kukiri ni kusema kama Mungu asemavyo katika maandiko.
Tunasema
kama Neno lisemavyo,tunasema Yesu alitufanyia nini msalabani, alipofufuka na
alipoketi mkono wa kuume. Tunasema sisi
ni nani kwake, yeye ni nani kwetu, tunasema tuna kitu gani ndani yake, tunasema
kama Neno lisamavyo. Imani ya Neno la Mungu huanzia mioyoni mwetu
na utimilika vinywani mwetu. Imani hii iwapo kinywani kwa njia ya maneno
tusemayo humwingiza Yesu kazini. Yesu amepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Anapata nafasi duniani kwa maneno yetu
yaliyosawa na Neno lake. Tunapotamka
maneno haya, mamlaka ya utendaji wake hujidhihirisha. Biblia inasema, “Basi iwapo tunaye kuhani mkuu
aliyeingia katika mbingu, Yesu mwana wa
Mungu na tuyashike sana
maungano yetu,” (Waebrania 4 :14). Tafsiri nyingine inasema, “Kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu kuliko wote
ambaye ameingia mbinguni, Yesu Mwana wa Mungu, basi na tushikamane sana kwa uthabiti na ule
ukiri wa imani yetu.” Tunaushika ukiri wetu, yaani maneno yetu
yalisemalo Neno lake
maana ameingia katika
mbingu kwaajili yetu, ayahudumie maungano yetu.
Imani
iliyopo moyoni husema kinywani. Kile
unachokijua kuhusu Mungu, kuhusu wewe katika Mungu au ushindi wako katika
Kristo utakisema kwa kinywa chako, pia utakitarajia kudhihirika kwa kuwa unaye
kuhani aliyesimama mbinguni kwaajili yako, ili adhihirishe maungano au maneno
yako ya imani. Kama alivyosema ni lazima
yatimizwe aliyoandikiwa (Luka 24:44), ni lazima ayatimize uliyoandikiwa wewe.
Thubutu kusema kama neno lisemavyo katika moyo
wako (Waebrania 13:5-6), atatimiza.
No comments:
Post a Comment