Thursday, April 2, 2015

Huduma ya Kikuhani ya Yesu



HUDUMA  YA  YESU  SASA
Msalaba ulifungua mlango wa Yesu kuingia mbinguni kufanya huduma ya Kikuhani. Msalabani Yesu alijitoa sadaka, mbinguni Yesu anatuhudumia kwa sadaka aliyoitoa msalabani.
I. HUDUMA YA KIKUHANI NI NINI?
Hii ni huduma inayohusisha mambo yafuatayo:
1. Uwakilishi kwa Damu yake2.Uunganishi kwa damu yake 3. Kumkaribia Mungu kwa damu yake 4. Kuwashika watu na Mungu na kuwaweka pamoja kwa njia ya sadaka yeke mwenyewe.                                 
II. AINA ZA UKUHANI
1. Ukuhani wa Haruni
Huu ulikuwa ni ukuhani wa mfano wa ukuhani wa kweli wa milele mbinguni. Ulitumia sadaka za wanyama. Patakatifu pa duniani, na mambo mengine ya kibinadamu.
2. Ukuhani wa Melikizedeki
Huu ni ukuhani halisi wa milele wa Yesu. Unatumia sadaka ya Yesu mwenyewe, patakatifu ni pa mbinguni, damu ya Mungu,huu ndio ukuhani halisi uliokamilika.
III. HUDUMA YA YESU WAKATI HUU
Huduma ya uwakilishi au uunganishi ya Yesu Kristo wakati wa sasa inaonekana kwa Yesu kuwa kama ifuatavyo:
MJUMBE (Mediator)
Yesu ni daraja la watu wote kumfikia Mungu. Binadamu wote hupitia kwake ili wakutane na Mungu (Yohana 14:6). Mtu anapotubu dhambi anatubu kupitia Yesu Kristo nasadaka yake aliyoitoa msalabani. Ni kama vile Yesu anamshika mtu huyo na kumuunganisha na Mungu, Yeye Yesu akiwa katikati (Ayubu 9:33, 1Timoteo 2:5, Waebrania 8:6).
MDHAMINI (Surety)
Yesu ni mdhamini wa agano jipya. Ni uhakika wa kutimia kwa agano jipya. Ahadi zote za Mungu katika agano jipya zimedhaminiwa na Yesu ili zitimie, dhamana yake ni Yesu na damu yake.  Kama vile mtu asipolipa pesa dhamana yake hukamatwa, agano limeshikwa kwa mdamini Yesu (Waebrania 7:22). Lisipotimia ‘Yesu atakamatwa’.

WAKILI (Advocate)
Yesu mbele za Mungu ni mtetezi wetu (1Yohana 2:1-3). Neno Mwombezi kwa Baba katika maandiko haya tafsiri yake ni wakili. Wewe kama mwamini ukikosea na kutubu dhambi, Yesu anasimama kama shahidi wa kusamehewa dhambi zako, maana alimwaga damu yake uokolewe.
MWOMBEZI (Intercessor)
Waebrania 7:25, inaonyesha Yesu ni mwombezi, Tafsiri rahisi ni anayekumbusha. Yesu anaweza kutuokoa kabisa, andiko hili ndivyo linavyosema. Tumeokolewa roho, tunafanywa upya nafsi, na siku moja miili yetu itabadilika. Yesu ndiye anayesimama mbele za Mungu kuhakikisha ukamilifu wetu umetimia, tunafanana naye kitabia, hata tutakapoingia mbinguni. Yeye anayatumia maneno yetu, ibada zetu, sifa, shukrani mbele za Mungu, UKIRI WA IMANI, hata udhihirisho utakapotokea duniani kwa neema.
                                                           (Waebrania 4:14-16)
WAKATI MWINGINE TUTAENDELEA KUMTAZAMA YESU KAMA KUHANI MKUU NA KUHANI WA ZAMU.

No comments:

Post a Comment