Tuesday, February 24, 2015

Mikononi Mwake



Hautoki Mkononi Mwake
“Wote anipao Baba watakuja kwangu; Wala yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe”
(Yohana 6:37)
Ikiwa umempa Yesu maisha yako, Mungu Baba amempa Yesu maisha yako. Ulipokwenda kwa Yesu na kumwamini, haikuwa wewe ilikuwa ni Mungu Baba anakupeleka kwa Yesu. Andiko lingine linasema, “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho. Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na Mungu. Basi kila aliyesikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu.” (Yohana 6:44-45).
Baada ya Yesu kukupa ufunuo ukamfahamu Yesu moyoni na kwenda kwake, Yesu anasema hakuna mtu awezaye kukutoa katika mikono yake Yesu.
Hakuna pepo, Shetani, jaribu, shida, malaika au kitu kingine chochote, kiwezacho kukutoa katika mikono ya Yesu. Kwa kuwa upo mikononi mwa Yesu upo salama. Fikiria hivyo, sema hivyo, waza hivyo.
Hakuna kitu kiwezacho kukutoa katika mikono ya Yesu, upo salama. HAUTOKI MIKONONI MWAKE.

No comments:

Post a Comment