SHUKRANI ZA KANISA
Maandiko yanaonyesha
shukrani alizoshukuru Paulo. Shukrani hizi zinaweza kuleta ongezeko katika kanisa na maisha
tunapozitumia. Kwa kushukuru namna hii tutakuwa tunafanya mapenzi ya Mungu, Maana shukrani ni mapenzi ya Mungu. Yesu alisema tuombe mapenzi yake yatimizwe. Shukrani hizi lazima zidhihirike, maana ni mapenzi ya Mungu.
1. Alishukuru kwakuwa Warumi Walikuwa watenda dhambi
wakatii Neema. Warumi 6:17 – 18 “ Lakini
Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa
mioyo yenu ile namna ya elimu ambayo mliwekwa chini yake; (18) na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa
watumwa wa haki.” Unaweza sasa ukamshukuru Mungu kwaajili ya kanisa au kwaajili
yako kwamba ulikuwa mtenda dhambi lakini sasa umeitii neema.
2. Shukuru imani yao inahubiriwa dunia yote. Warumi 1:8 “Kwanza namshukuru Mungu wangu katika Yesu
Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa kuwa imani yenu inahubiriwa katika dunia nzima.”
Unaweza kushukuru kwaajili ya imani yako ya wokovu, inahubiriwa, au inaweza kuhubiriwa
duniani pote.
3. Anatushangiliza daima. 2Wakorintho 2:14 “Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza
daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa
kazi yetu.”
4. Anatutia bidii. 2Wakorintho 8:16 “Lakini ahimidiwe Mungu atiaye bidii ile ile kwa ajili yenu katika moyo
wa Tito.” Shukuru kwakuwa Mungu anakushangiliza
daima. Katika hali zote zinazotokea unashangilizwa.
5. Wanalipokea Neno linatenda kazi. 1Wathesalonike 2:13 “Kwa sababu hiyo sisi nasi twamshukuru Mungu
bila kukoma, kwa kuwa, mlipopata ileneno la ujumbe la Mungu amlilolisikia
kwetu, mlilipokea si kama neon la wanadamu, bali kama neno la Mungu; na ndivyo
lilivyo kweli kweli, litendalo kazi pia ndani yenu ninyi mnaoamini.” Shukuru
kwakuwa Neno la Mungu unalolipokea linatenda kazi. Ikiwa wewe ni muhudumu wa Neno
shukuru kwa Neno unalosema kwa watu wako kwamba linatenda kazi.
6. Mungu amewachagua tangu mwanzo wapate wokovu katika
kutakaswa na Roho. 2Wathesalonike 2:13 “
Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu
mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu,
katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli.” Shukuru kwaajili yako na kanisa
kwamba Mungu amewachaagua tangu mwanzo, mpate wokovu katika kutakaswa na Roho.
7. Omba na kushukuru kwa macho ya kiroho kufunguka na kuelewa mambo ya kiroho. Waefeso
1:15 – 23 “ Kwa sababu hiyo mimi nami,
tangu nilipopata habari za imani yenu katika Bwana Yesu, na pendo lenu kwa
watakatifu wote, (16)siachi kutoa
shukrani kwa ajili yenu; nikiwakumbuka katika sala zangu, (17)Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape
ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; (18)macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito
wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu
jinsi ulivyo; (19)na ubora wa ukuu wa
uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za
uweza wake; (20)aliotenda katika
Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa
roho; (21)juu sana kuliko ufalme wote, na
mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humutu,
bali katika ule ujao pia; (22)akavitia vitu vyote
chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa;
ambalo (23)ndilo mwili wake, ukamilifu wake
anayekamilika kwa vyote katika vyote.”
No comments:
Post a Comment