Saturday, December 13, 2014

Neema Yatutosheleza


Utoshelevu Wetu ni Yeye
Mungu ametutosheleza kuwa wahudumu katika Agano jipya. Huduma ni utekelezaji wa kusudi fulani linalofanyika ndani ya Yesu kwa uwezo wa Roho wake, ili kujaza pengo fulani, au kutatua tatizo fulani. Kwa mfano kufanya kazi na kutoa sehemu ya mapato yako, kuwafikia wasiofikiwa na injili, hiyo ni huduma, umetatua tatizo kwa sehemu la kutofikiwa na injili.  Hiyo kazi yako au biashara ione kama ni huduma. Iombee ikirie Neno kama anavyoomba muhubiri kabla ya kufanya huduma yake ya kuhubiri.

Unapofundisha Neno, unatatua tatizo la watu kutojua Neno, hapo unahudumu. Unapofanya maombezi unaziba pengo la watu kutolindwa au kutokuwa na neema ya kutimiza huduma zao hapo unafanya huduma. Unaposhuhudia watu waokoke, unaziba pengo, unatatua tatizo la watu kwenda jehanam. Unapotembelea mtu mwenye shida unatatua tatizo la kukata tamaa nk! Unaposifu na kuabudu, unajaza pengo lisilojaa milele! La moyo wa Mungu kutaka kusifiwa na kuabudiwa, hapo unahudumu.
Katika huduma yoyote ufanyayo utoshelevu, au uwezesho wa kuweza kuitimiza sio wa kwako, bali watoka kwa Bwana. Kwa njia ya Roho wake wewe ni muhudumu wa Agano jipya. Hutumii nguvu zako na Sheria ya Musa bali nguvu za Roho. Katika huduma au tatizo lolote uliloumbwa katika Yesu ulitatue kumbumka utoshelevu wako watoka kwake, sema hivyo, ombea huduma hivyo. Maandiko yaliyofafanuliwa yanasema: 

Ni Yeye Bwana aliyetufanya tustahili na tuweze, kama wahudumu wa Agano Jipya, Sio wa andiko la sheria, kwali kwa Roho Mtakatifu anayehuisha.” (2Wakorintho 3:6)

No comments:

Post a Comment