Wednesday, November 19, 2014

Huduma ya Mtume


   Aina za Huduma
Kwaajili ya kuelewa vizuri tutaangalia huduma katika makundi matatu
1.   Huduma za viongozi (karama za Yesu)
2.   Huduma za masaidiano
3.   Huduma za kanisa
Huduma za Uongozi
Huduma hizi zipo tano ni Yesu mwenyewe huzitoa, ni karama za Yesu.  Karama za Roho hazipo wakati wote huja kwa uhitaji maalumu, lakini hizi ni ofisi za wakati wote.
1.   Mitume (Apostolos)

(a)  Aliyetumwa kuwakilisha ufalme kama balozi
(b)  Ni mwanzilishi na mweka msingi wa kanisa jipya au makanisa mapya, huweka msingi kwa kufanya yafuatayo:
(1)  Huhubiri  (2) Hufundisha (3) Hufunza viongozi wapya (4) husimamia mafundisho sahihi ya Imani.
(c)  Mara nyingi huanza kwa kupitia huduma nyingine na yenyewe ya kitume kuonekana baadaye (Matendo 13:1-3). Mtume lazima awe amekuwa kiroho na kihuduma, kabla ya kuanza utume. Mfano TL Osborn alikuwa mchungaji kabla ya utume. Reinherd Bonnke alikwa Mchungaji kabla ya uinjilisti wa kimishionari. Paulo alikuwa mwinjilisti na mwalimu kabla ya kuanza utume (Matendo 13).
(d)  Mitume huitwa na Yesu na kupelekwa na kanisa.
Aina za Mitume
(1)  Mitume 12 (mitume wa mwanakondoo)
(2)  Mitume wa kupaa (Walioitwa baada ya Yesu kupaa,Waefeso 4:10-13). Hoja kwamba leo hakuna mitume ni uongo, maana uhitaji wa injili kufika maeneo yasiyofikiwa ni mkubwa kuliko wakati wowote.
(3)  Mitume wa uongo
(e)  Mitume hufanya kazi ya kimishionari, huvuka mipaka ya kitamaduni na kuhubiri injili, huanzisha makanisa, kuandaa na kuweka viongozi maeneo tofauti na utamaduni wao, kama vile lugha nk.
(f)   Karama kuu zifanyazo kazi pamoja na huduma katika huduma hii ni ualimu, uinjilisti, miuijiza, usimamizi (maongozi) na hufanya kazi karibu na manabiii au wao wenyewe mitume huwa manabii. 
(g) Mtume lazima awe mwinjilisti, huduma ya mwinjilisti hufanya kazi karibu na mtume. Naweza kusema hakuna mtume asiye mwinjilisti. Katika hali ya kidini huduma ya mwinjilisti imedharauliwa, lakini ni huduma muhimu sana agano jipya, maana ni agano la injili ya Yesu Kristo.
(h) Huduma hii haipo kwa wanaume tu, ni kweli mitume wa mwanakondoo, wale 12 walikuwa wanaume tu. Baada ya Yesu kupaa alitoa mitume wengine wanaume kwa wanawake; mfano Warumi 16:7, inaonyesha mtume mwanamke aliyeitwa Yunia.
(i) Dalili nyingine ya huduma hii, mitume huwa mababa wa viongozi wengi wa kiroho, kwa mfano Paulo alikuwa baba wa viongozi wengi wa kiroho, kwa mfano wa Mozes Kulola.

No comments:

Post a Comment