Mwombaji wa Utimilifu
Wewe
kama mwombaji wa maombi ya utimilifu yakupasa ufahamu mambo yafuatayo:
Omba
Ukiwa katika Nafasi yako ya Mtoto wa Mungu
Unapomwendea
Mungu kuomba maombi ya utimilifu nenda kama
mtoto wake uliyekubaliwa naye, kwa njia ya Kristo Yesu. Paulo alimwendea Mungu kama
Baba, “…nampigia Baba magoti,” (Waefeso
3:14)
Fahamu ya kuwa Mungu Baba anakusikia kwa kuwa ni mtoto wake.
Omba
Ukiwa na Ujasiri
Fahamu
ya kuwa maombi ya utimilifu ni maombi yaliyo sawa na Neno la Mungu. Neno lake ni
mapenzi yake. Kufahamu ya kuwa unaomba kama Mungu atakavyo yaani unapo omba katika mapenzi yake,
unakuwa na ujasiri wa imani katika kupokea, “Na huu ndio ujasiri tulionao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na
mapenzi yake, atusikia.” (1 Yohana 5:14).
Kwa upande mwingine ujasiri wetu mbele zake katika maombi unatokana na
maisha ya kumpendeza tunayoishi mbele zake. Haya ni maisha ya kulitenda Neno
lake, maandiko yanasema,”Wapenzi, mioyo
yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa
Mungu; na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake” (Yohana
3:21-22).
Omba
kwa Bidii
Omba
kwa kumaanisha, usitamke maneno
matupu mbele za Mungu, sema maneno
yaliyoushika moyo wako, ambayo yako sawa na Neno la Mungu. Omba kwa kung’ang’ania, usiwe mwepesi
kuondoka mbele za Mungu. Maombi yako
usemayo mbele zake yawe kama ni uhai wako mwenyewe, yaani kama
sehemu ya maisha yako. Maombi ya namna
hii ni maombi ya bidii, mara nyingine maombi haya huambatana na machozi au
kufunga, ukiyafanya kama mtu mwenye haki utapokea, “…Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana,
akiomba kwa bidii.” (Yakobo 5:16).
Omba
kwa Jina la Yesu
Omba
kwa kutumia Jina la Yesu, omba kwa kibali na mamlaka aliyokupa Yesu mbele za
Baba, yaani Jina lake, “…Mkimwomba Baba
neno lolote atawapa kwa jina langu.” (Yohana 16:23). Tegemea kuona matokeo katika maisha yako na Kanisa
baada ya kuanza kufanya maombi na maombezi ya utimilifu.
Sentesi
zifuatazo zinaonyesha kwa kifupi maombi ya utimilifu:
Baba kwa jina la Yesu ninaomba
unisimamishe imara katika mapenzi yako yote, Nifanye imara moyo wangu niweze kutenda mema katika utimilifu wote
yaani, nisifanye lolote lililo baya.
Nguvu za Roho Mtakatifu ziambatane
nami wakati wote katika huduma. Ninakuomba Baba pendo lako ndani yangu
lizidi katika hekima yote na ufahamu wa
rohoni. Pia ninaomba haya kwa kanisa
lako na watumishi wako wote, ili watimilike katika kutenda mapenzi yako,
kutenda mema,katika nguvu zako na katika pendo linalotuunganisha na kutupa
umoja. Kwa jina la Yesu, Amina.
Ikiwa kitabu hiki kimekupa hatua mpya au una
swali lolote usisite kuwasiliana nami kwa anuani na simu zilizopo mwanzoni mwa
kitabu. Pia ni vizuri kama
utaweza kupata vitabu vingine ambavyo nimeviandika kwa msaada wa Mungu ili
ujengwe kiroho.
Ikiwa
unapenda kuwa mwombaji na kuombea utimilifu lakini bado haujampa Yesu Maisha
yako sema sala Hii:
Mungu Baba
ninkuja kwako kwa jina la Yesu, naomba unisamehe dhambi zangu. Yesu Mwokozi ingia ndani yangu, uwe Bwana na
Mokozi wangu, naamini ulikufa na kufufuka, ili kwa damu yako nitakaswe na
kuhesabiwa haki, nisiingie katika hukumu ya Mungu. Ninakushukuru Baba kwa jina la Yesu, Amina.
No comments:
Post a Comment