Kuachilia Roho Njema
Maneno
hutenda kazi moja kwa moja na roho. Siwezi kuiona roho yako, lakini naweza
kuiona unapoongea. Maandiko yanaonyesha maneno na roho hufanya kazi kama kitu kimoja. Katika Yohana 6:63, Yesu alisema maneno
yake ni roho tena ni uzima. Mithali 18:21, inaonyesha mauti na uzima huwa
katika uwezo wa ulimi, mauti ni roho na uzima ni roho, zote hufanya kazi kwa
ulimi. Ezekieli 2:2 inaonyesha Mungu aliposema na Ezekieli roho ikamwingia.
Matendo ya Mitume 10:44, Petro aliposema Neno Roho aliwashukia waliomsikiliza.
Yohana 20:22, Yesu aliwavuvia Roho wanafunzi kwa kusema neno.
Aina ya Roho
na Hali ya Moyo
Hali
ya moyo inaweza kuachilia aina ya roho fulani. Moyo wenye huzuni huachilia roho
ya huzuni. Moyo wa woga huachilia roho ya woga. Moyo wa upendo huachilia roho
ya upendo. Moyoni hutoka chemchemi nzuri au mbaya ambazo ni roho. Hutoka kwa
njia ya maneno. Isaka, Moyo wake ulipofurahi aliachilia maneno ya baraka yenye
roho ya baraka (Mwanzo 27:1-4, 27,28). Nuhu moyo wake ulipokasirika aliachilia
maneno ya laana yenye roho ya laana (Mwanzo 9:24).
Maneno
Yasemwapo Huendelea Kuwepo
Maneno
yanapotamkwa hugeuka kuwa roho na kuendelea kuwepo, au huachilia roho
inayotenda. Ukimsema mtu vibaya kwa moyo wa chuki au wivu, unakuwa unamzunguka
kwa maneno hayo, kisha roho ya maneno hayo huanza kupigana naye. Maneno
yanapigana kwa roho. Maandiko yanasema, “Naam,
kwa maneno ya chuki wamenizunguka, wamepigana nami bure.” (Zaburi 109:3).
Ukiamua
unaweza kumzunguka mtu na maneno mazuri au mabaya. Wakati wa maombezi ni muhimu
kwanza usikie kumpenda mtu unayemwombea. Baada ya kusikia hivyo ukianza kuomba
utaachilia maneno yanye roho njema itakayomzunguka na kuleta mambo mema.
Mara
nyingine ukihisi kutamkiwa maneno mabaya, au ukiyasikia, tamka maneno mazuri kama Neno lisemavyo ili kuachilia roho njema. Ukiaa kimya
maneno hayo yanaweza kukuzunguka na roho mbaya zikapigana nawe.
Jizungushie
Roho Njema
Roho ya
Ulinzi
Jizungushie
roho ya ulinzi kwa kusema Bwana ni mwaminifu atakufanya imara na kukulinda na
yule mwovu (2 Wathesalonike 3:3). Sema Bwana atakulinda na mabaya yote na
kukuhifadhi mpaka utakapoingia mbinguni (2Timoteo 4:18).
Roho ya
Ushindi
Katika
hali zote sema unako kushinda kwa Yesu Kristo (1Wakorintho 15:57).Katika yote
unashinda (Warumi 8:37).
Mara
zote jizoeshe kuzungushia wengine roho njema kwa njia ya Neno la Mungu. Hii
uifanye ukiwa na moyo wa furaha, amani na upendo. Utaleta hali ya hewa ya
mbinguni kwako na wenzio.
Katika
anga la Tanzania
kuna manung’uniko mengi yanayoachilia roho mbaya. Ukisikia watu wanalalamikia
kitu fulani juu ya nchi au Serikali, uwe karibu na Roho akuwezesha kuachilia
roho njema katika mazingira hayo. Hii pia inaweza kufanyika kanisani, katika
familia nk.
No comments:
Post a Comment