Haujui Ufanyeje Unapo
pa Kutazama
“…Wala
hatujui tufanyeje; ila macho yetu yanatazama kwako” (2 Nyakati 20:12)
Mfalme Yehoshafati alizungukwa na maadui. Katika maombi yake kwa Mungu alimwambia,
hajui afanyeje ila macho yake yalielekea kwake. INGAWA HAKUJUA AFANYEJE, ALIJUA
ATAZAME WAPI.
Alikuwa napo pa
kutazama, ingawa hakujua cha kufanya. Aliposema macho yetu yatazama KWAKO, neno hili kwako,
linawakilisha nafsi ya Mungu. Katika
agano jipya macho yetu yanatazama kwa Yesu. Yanatazama nafsi ya Yesu tu, katika hali zote zinazotuzunguka. Yeye alifanyika
mwili akakaa kwetu, ni mfano wa Mungu asiyeonekana aliyeombwa na Yehoshafati.
Usomapo Injili: Yohana, Marko, Luka na Mathayo na ukakutana
na maneno aliyosema Yesu yenye neno: mimi,
langu, wangu, kwangu, au nami, maneno haya yanaonyesha nafsi ya Yesu ambayo
yatupasa tuitazame hata kama hatujui
tufanyeje, IWE NI SHABAHA TUSIIPOTEZE NA KUTAZAMA KITU KINGINE. Vita kuu ya
ibilisi ni kututoa macho yetu kwake, macho yetu kuwa kwake ni wokovu
kwetu. Mifano ionyeshayo nafsi ya Yesu katika utendaji:
1. Mimi nilikuja
ili wawe na uzima…(Yohana 10:10) 2. Njooni kwangu
ninyi nyote…(Mathayo 11:28) 3. Kwa jina langu…(Marko
16:17) 4. Juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa
langu (Mathayo 16:16-19) 5. Nami
nawapa uzima wa milele wala hawatapotea… (Yohana 10:28). 6. …wala hana kitu kwangu (Yohana 14:30).
Katika hali yeyote uliyonayo itazame nafsi ya Yesu kwa
maandiko kama haya yanavyoionyesha. Hata kama hujui ufanyeje. Katika asaya
45:22, Mungu anasema niangalieni mimi mkaokolewe. Yehoshafati alimwangalia Yeye
akaokolewa. Waebrania 12:2, inasema
tukimtazama yeye aliyeanzisha na mwenye kutimiza imani yetu, yaani Yesu. Kwa
kuwa yeye ni Mungu pamoja nasi (Mathayo 1:23), tumtazamapo tutaokolewa katika
hali zote kama alivyosema katika Isaya 45:22.
Maandiko yanasema, “Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki
mwito wa mbinguni, mtafakarini sana mtume na kuhani mkuu wa maungamo yetu Yesu.”
(Waebrania 3:1). Unaweza ukawa hujui ufanyeje, lakini unaye wa kumtafakari.
Kutafakari ni kutazama kwa ndani.
Tafakari jinsi alivyokupenda. Jinsi alivyoondoa dhambi zako, jinsi
alivyomshinda Shetani kwaajili yako, jinsi anavyokuandalia makao mbinguni,
jinsi alivyoshinda magonjwa na mashetani kwaajili yako, alipokuwa duniani.
Tafakari/mtazame yupo ndani yako, ikiwa umempokea! Hajabadilika yupo vile vile
kama zamani (Matendo 13:8). Kama mashetani yalivyomwogopa (Marko 1:23-25),
ndivyo yanavyomwogopa sasa akiwa ndani yako. Sema kwa kinywa chako huku ukiitaja hali yako “Sijui
nifanyeje, ninapo pa kutazama:
YESU AITWAYE KRISTO”
No comments:
Post a Comment