Friday, June 13, 2014

Hana Kitu Kwangu



Hana Kitu Kwangu
Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu wala hana kitu kwangu”
(Yohana 14:30)
Yesu anasema hapa, mkuu wa dunia, yaani Shetani, anakuja kwake na hana kitu kwake. Mkuu huyu anayetajwa hapa katika tafsiri ya msingi ni mjanja, mwovu, mwenye hila na mwenye akili.  Anakuja katika nafsi ya Yesu, lakini hana kitu kwake.
Hana Kitu
Yesu anasema Shetani hana kitu kwake, kwa maana ya: Hawezi kumshika, hawezi kushirikiana naye, hawawezi kuwa pamoja. Yesu na Shetani hawako pamoja, Shetani hawezi kukaa na Yesu wala kumkaribia.
Yesu Yupo Ndani Yako
Mahali pengine Yesu anasema anasimama mlangoni anabisha na mtu akisikia sauti yake ataingia na watakula wote (Ufunuo 3:20). Kula na Yesu ni kushirikiana naye, ni kushiriki nafsi yake na hali yake. Kushiriki nguvu iliyomfufua, upendo wake, uwezo wake, tabia yake nk.  Pia kushiriki mamlaka yake dhidi ya Shetani, ambayo imemfanya Shetani ashindwe kukaa naye. ‘Ukristo’ yaani wokovu ni Kristo pamoja nasi ni kumshiriki Kristo ni  kula pamoja naye.
Mfano wa ushirika wako na Kristo ni  unaonekana kwa njia ya Mzabibu(Yesu) na tawi (wewe), (Yohana 15:1-5). Umeshiriki nafsi ya Yesu, kutoka kwake unazaa matunda. Umeshiriki nguvu iliyomtoa kaburini kwa hiyo unazaa matunda.  Sasa wewe na Yesu ni umoja.  Shetani hana kitu kwako kwa njia ya Yesu aliye ndani yako.
SEMA: Kwa Yesu aliye ndani yangu Shetani hana kitu kwangu. Kama alivyo sasa mbinguni niko hivyo duniani. Ananiwakilisha mbinguni kama Kuhani na mfalme, namwakilisha duniani kama Mfalme na Kuhani. Kwa ushuhuda huu ninashinda tena leo! (Shirikisha watu wengine ushuhuda huu, hasa katika ibada ya nyumbani.)

1 comment: