I
KUJA KWA ROHO MTAKATIFU
Roho Mtakatifu ni Mungu,
na ujio wake ulitabiriwa toka Agano la Kale. Ukaanza kuonekana kwa Kristo Yesu
kama malimbuko, mwishoni ukadhihirika ndani ya kanisa lake ambalo ni mwili
wake. Anaitwa ni Roho wa Ahadi, aliahidiwa.
ROHO
NA YESU
Katika Agano la Kale
maandiko yanasema, “Roho ya Bwana MUNGU i
juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari
njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao
na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao. (2) Kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu
wetu; kuwafariji wote waliao.” (Isaya 61:1-2)
Maandiko haya ya Isaya
yalitimia Agano Jipya juu ya Yesu Kristo, alisema Yesu akinukuu maandiko haya, “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana
amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia
wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru
waliosetwa. (19) Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa” (Luka 4:18,21).
Roho Mtakatifu anaonekana kupitia Yesu Kristo. Huwezi kumtaja Roho na kumpata
Roho bila Yesu. Kuja kwa Roho Mtakatifu msingi wake ni kuja kwa Masihi yaani Yesu,
na Roho huyo kuwa juu ya Yesu. Kila mtu atakaye kumpokea Roho lazima ajue
anampokea tokea kwa Yesu.
DUNIA
NA ROHO MTAKATIFU
Katika Agano la Kale
kitabu cha Yoeli 2:28, maandiko yanaonyesha unabii wa Roho Mtakatifu kumwagwa
duniani. Unabii huu ulitimia katika Matendo ya Mitume 2:1-4, imeandikwa, “(1) Hata ilipotimia siku ya Pentekoste
walikuwako wote mahali pamoja. (2)
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kwa
kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. (3) Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia
kila mmoja wao. (4) Wote wakajazwa
Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia
kutamka.” Maandiko katika mstari wa 16 – 21 wa sura hii na yanaendelea
kuelezea unabii ule wa Yoeli 2:28-32.
Kipindi hiki tulichopo ni
kipindi cha Roho Mtakatifu ameshamwagwa duniani ni kipindi cha kupokea Roho
Mtakatifu aliyekwisha tolewa. Yoeli mlango wa pili ilikuwa inaonyesha unabii wa
Roho Mtakatifu kuja, Matendo mlango wa pili inaonyesha kutimia kwa unabii huo
kupitia Yesu Kristo.
No comments:
Post a Comment