Wednesday, March 11, 2015

Kushukuru!



KUMSHUKURU MUNGU
I.            KUMSHUKURU NI NINI?

1.    KUJALI
Luka 17:15 – 16 “Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu; (16)Akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

2.    KUTUKUZA
Luka 17:17 – 19 “Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi? (18)Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu? (19)Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.
Zaburi 50:23 “Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza.”

3.    KUTOA SADAKA YA KINYWA “Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani.” Yona 2:9 “Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa BWANA.”

4.    ISHARA YA KUMJUA MUNGU
Warumi 1:21 “kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza; kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.

II.         KUANDAA MOYO WA SHUKRANI

1.    TAFAKARI FADHILI ZAKE
v  Fadhili ni vitu alivyotoa kwa rehema zake
Zaburi 106:1 – 2 “Haleluya. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake ni za milele. Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya BWANA, Kuzihubiri sifa zake zote?
Mfano:
a)    Alikuchagua katika Kristo
b)   Alikuita
c)    Akakuokoa
d)   Akakutia muhuri wa Roho
e)    Nk.
Zaburi 111:1 – 2 “Haleluya. Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote, Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano. Matendo ya BWANA ni makuu, yafikiriwa sana na wapendezwao nayo.

III.       KWA MOYO WOTE
Zaburi 103:1 – 2 “Ee nafsi yangu, umhimidi BWANA. Naam, vyote vilivyo ndani yangu vilihimidi jina lake takatifu. Ee nafsi yangu, umhimidi BWANA, Wala usizisahau fadhili zake zote.”
Mhimidi (mbariki) na vyote vilivyomo ndani yangu vilihimidi jina lake takatifu”
…………….. Mhimidi Bwana wala usizisahau fadhili zake……..(Do not forget his benefit”
Zaburi 111:1 – 2 “Haleluya. Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote, Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano. Matendo ya BWANA ni makuu, yafikiriwa sana na wapendezwao nayo.
IV.        NAMNA YA KUSHUKURU

1.    SHUKURU KWA ALIYOKWISHA FANYA: Unaweza kuanza kushukuru kwa mambo yaliyokwisha pita aliyokufanyia katika maisha au kazi ya Yesu  msalabani.
v  Alimtoa Yesu
v  Alikuvuta kwa Roho ukazaliwa mara ya pili
v  Alikulinda toka utoto
v  Hakuacha ufe kabla hujaokoka
v  Aliandaa wokovu wako toka bustani ya Edeni (Mwanzo 3:15)

2.    KUSHUKURU KWA ULIYONAYO SASA: Shukuru kwaajili ya mambo yaliyopo sasa. Unapoona huna kitu fulani tafuta hapohapo ulichonacho na kushukuru.
1.    Mfano; ukiwa hujafika form four, shukuru kwa kuwa umefika darasa la saba
2.    Ikiwa huna mtoto shukuru sababu una kizazi
3.    Ikiwa mguu mmoja unauma shukuru sababu wa pili hauumi
4.    Ikiwa huna chakula shukuru unalo jiko
5.    Utagundu vitu ulivyonavyo alivyokupa Mungu ni vingi kuliko usivyonavyo.
6.    Shukuru kwa jina la Yesu (Waefeso 5:20) “na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo”

3.    SHUKURU KWA YATAKAYOTOKEA:Shukuru kwaajili ya mambo yajayo, unayotarajia kuyaona kabla hujayaona.
1.  Shukuru kwa majibu ya maombi uliyoomba, kabla ya kuyaona.
2.  Shukuru kwaajili ya ahadi Mungu alizosema na zinaenda kutokea. Kwa mfano katika jaribu shukuru kwa kutumia ahadi ifuatayo maishani mwako:
1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

Katika ushindani wa kiroho unapoona mashambulizi ya kishetani, shukuru kwa ahadi ifuatayo: Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Katika huduma na udhihirisho wa nguvu za Mungu tumia, Marko 16:15 – 20 “Akawaambia, enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri injili kwa kila kiumbe.(16)Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. (17)Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; (18)watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya. (19)Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. (20)Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja na kulithibitisha lile neon kwa ishara zilizofuatana nalo.”

SIYO AHADI HIZI TU,  BALI NA NYINGINE PIA. SHUKURU KWA AHADI KANAKWAMBA ZIMESHATIMIA MAISHANI MWAKO

V.           FAIDA ZA SHUKRANI

1.    SHUKRANI INASIMAMISHA IMANI
Imani hupokea sasa na kuyaona ndani mambo yanayotarajiwa kuonekana nje baadaye. Shukrani ni tendo la imani linaloonyesha umeshapokea sasa. Pasipo matendo imani haizai, shukrani ni tendo linaloizalisha imani“Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutoamini bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu  Warumi 4:20

2.    SHUKRANI INATAKASA
Luka 17:17 – 19 “Yesu akajibu, akanena Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi? (18) Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu? (19) Akamwambi, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.”1Timotheo 4:1 – 5
·         Kusafisha
·         Kutenga
Mwenye ukoma alipoenda kushukuru kwa Yesu, alitakasika kabisa, siyo kupona tu. Tunaposhukuru kwaajili ya chakula kinatakaswa. Kinatengwa maalum kwaajili ya utukufu wa Mungu.
3.    SHUKRANI INAZIDISHA
Yohana 6:1 – 13 “Baada ya hayo Yesu alikwenda zake ng’ambo ya Bahari ya Galilaya, nayo ndiyo ya Tiberia.(2)Na mkutano mkuu wakamfuata, kwa sababu waliziona ishara alizowafanyia wagonjwa. (3)Naye Yesu akakwea mlimani, akaketi huko pamoja na wanafunzi wake. (4)Na Pasaka, sikukuu ya Wayahudi, ilikuwa karibu. (5)Basi Yesu alipoinua macho yake akaona mkutano mkuu wanakuja kwake, alimwambia Filipo, Tununue wapi mikate, ili hawa wapate kula? (6)Na hilo alilinena ili kumjaribu; kwa maana alijua mwenyewe atakalotenda. (7)Filipo akamjibu, Mikate ya dinari mia mbili haiwatoshi, kila mmoja apate kidogo tu. (8)Wanafunzi wake mmojawapo, Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia, (9)Yupo hapa mtoto, yuna mikate mitano ya shayiri na samaki wawili, lakini hivi ni nini kwa watu wengi kama hawa? (10)Yesu akasema, Waketisheni watu. Na mahali pale palikuwa na majani tele. Basi watu waume wakaketi, wapata elfu tano jumla yao. (11)“Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka. (12)Nao waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kisipotee cho chote. (13) Basi wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili, vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyowabakia wale waliokula.” Baada ya Yesu kushukuru mikate na samaki viliongezeka. Unaposhukuru kwa mambo machache ni rahisi kuongezeka.
4.    SHUKRANI INAKUOKOA NA KUNUNG’UNIKA
1Wakorintho 10:1 – 12 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; (2)wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; (3)wote wakala chakula kile kile cha roho; (4) Wote wakanywa kinywaji kilekile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba war oho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. (5)Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani. (6)Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. (7)Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze. (8)Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. (9)Wala tumjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka. (10)Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu. (11)Basi mambo hayo yote yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. (12)Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.” Badala ya kunungunika kwaajili ya mambo yanayokuhusu, shukuru. Shukkrani inaondoa manunguniko na kukufanya uendelee kumfurahia Mungu.

5.    SHUKRANI INAFUFUFA NA KUONDOA HARUFU MBAYA
Yohana 11:38 – 44“Basi Yesu, hali akiugua tena nafsini mwake, akafika kwenye kaburi. Nalo lilikuwa na pango, na jiwe limewekwa juu yake. (39)Yesu akasema, liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne. (40)Yesu akamwambia, mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu? (41)Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia. (42)Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia siku zote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma. (43) Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. (44)Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akamwaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.”.  Baada ya Yesu kushukuru Lazaro alifufuka kwa kuamuru. Msiba uliisha! Maiti iliyoanza kunuka ikaacha. Hali hata ikiwa imechafuka tushukuru na kutamka mapenzi ya Mungu kwa kuamuru.

6.    SHUKRANI NI MAPENZI YA MUNGU
1Wathesalonike 5:18 “shukuru kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.”
1Yohana 5:14 “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.”
Wakolosai 4:2 “Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani”. Kuomba twaomba kwa mapenzi ya Mungu, tunaposhukuru tunafanya mapenzi ya Mungu.

7.    SHUKRANI ZINAENENDA NA USAFI WA DHAMIRI
2Timotheo 1:3 “Namshukuru Mungu, nimwabuduye kwa dhamiri safi tungu zamani za wazee wangu, kama vile nikukumbukavyo wewe daima, katika kuomba kwangu usiku na mchana.”. Shukurani zinatunza dhamiri safi.
VI. JINSI YA KUSHUKURU
1.    Kwa kushangilia moyoni. Luka 10:21 “Saa ile ile alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; naam, Baba kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza.

2.    Shukuru kwa jina la Yesu. Waefeso 5:20 “namshukuru MunguBaba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo

3.    Shukuru kwa maneno na kuimba

4.    Shukuru kwa sadaka
VII. SHUKRANI ZA KANISA (ONGEZEKO)
Maandiko yanaonyesha shukrani alizoshukuru hasa Paulo. Shukrani hizi  zinaweza kuleta ongezeko katika kanisa na maisha tunapozitumia.
1.    Alishukuru kwakuwa Warumi Walikuwa watenda dhambi wakatii Neema. Warumi 6:17 – 18 “ Lakini Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa mioyo yenu ile namna ya elimu ambayo mliwekwa chini yake; (18) na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki.” Unaweza  sasa ukamshukuru Mungu kwaajili ya kanisa au kwaajili yako kwamba ulikuwa mtenda dhambi lakini sasa umeitii neema.

2.    Shukuru imani yao inahubiriwa dunia yote. Warumi 1:8 “Kwanza namshukuru Mungu wangu katika Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa kuwa imani yenu inahubiriwa katika dunia nzima.” Unaweza kushukuru kwaajili ya imani yako ya wokovu, inahubiriwa, au inaweza kuhubiriwa duniani pote.

3.    Anatushangiliza daima. 2Wakorintho 2:14 “Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.”
4.    Anatutia bidii. 2Wakorintho 8:16 “Lakini ahimidiwe Mungu atiaye bidii ile ile kwa ajili yenu katika moyo wa Tito.”  Shukuru kwakuwa Mungu anakushangiliza daima. Katika hali zote zinazotokea unashangilizwa.

5.    Wanalipokea Neno linatenda kazi. 1Wathesalonike 2:13 “Kwa sababu hiyo sisi nasi twamshukuru Mungu bila kukoma, kwa kuwa, mlipopata ileneno la ujumbe la Mungu amlilolisikia kwetu, mlilipokea si kama neon la wanadamu, bali kama neno la Mungu; na ndivyo lilivyo kweli kweli, litendalo kazi pia ndani yenu ninyi mnaoamini.” Shukuru kwakuwa Neno la Mungu unalolipokea linatenda kazi. Ikiwa wewe ni muhudumu wa Neno shukuru kwa Neno unalosema kwa watu wako kwamba linatenda kazi.

6.    Mungu amewachagua tangu mwanzo wapate wokovu katika kutakaswa na Roho. 2Wathesalonike 2:13 “ Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli.” Shukuru kwaajili yako na kanisa kwamba Mungu amewachaagua tangu mwanzo, mpate wokovu katika kutakaswa na Roho.

7.    Omba na kushukuru  kwa macho ya kiroho  kufunguka na kuelewa mambo ya kiroho. Waefeso 1:15 – 23 “ Kwa sababu hiyo mimi nami, tangu nilipopata habari za imani yenu katika Bwana Yesu, na pendo lenu kwa watakatifu wote, (16)siachi kutoa shukrani kwa ajili yenu; nikiwakumbuka katika sala zangu, (17)Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; (18)macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; (19)na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; (20)aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; (21)juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humutu, bali katika ule ujao pia; (22)akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo (23)ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.
JENGA KANUNI HIZI
1.    Usifikiri ambayo huna shukuru kwa uliyonayo

2.    Angalia mambo ya milele aliyokufanyia Mungu siyo ya muda mfupi
Ukishukuru unafanya mapenzi ya Mungu. 1Wathesalonike 5:18. “shukuru kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” (Hukosei)

3.    Katika hali zote Mungu anaweza tokeza jema hivyo shukuru. Warumi 8:28“ Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.

No comments:

Post a Comment