Monday, January 26, 2015

Usiache Kukiri Imani




UKIRI WA IMANI
I. IMANI NI NINI? (Waebrania 11:1), “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo…”.  Kwa maneno mengine tafsiri hii inasema, “ Basi imani ni uhakika, ni hati miliki ya vitu tunavyovitarajia vidhihirike”. Imani ni hati miliki ya moyoni, unayo hata kama mwilini huoni ulichomiliki, lakini ndani tayari unacho na una uhakika wa kuona udhihirisho wa kutokea kwake kwa nje.
A.    Imani ni kumiliki sasa mambo yanayoenda kudhihirika kwa kuonekana
B.    Imani ni kupokea sasa kitu kitakachoonekena baadaye au muda mfupi ujao.
C.    Imani ni msingi wa mambo yatakayodhihirika (hupostasis). Bila msingi huo hayadhiriki.
D.    Kabla ya jambo kudhihirika uhakika wa udhihirisho wake ni neno la Mungu. Neno hili huzaa uhakika huo moyoni, huwa ni msingi wa kudhihirisha litarajiwalo.
E.    Imani ni uhakika wa moyoni wa unaopokea sasa na kujenga tumaini akilini la kuona udhihirisho wakati ujao.
F.    Kabla ya udhihirisho imani ya moyoni au uhakika wa moyoni, huomba, hushukuru, husifu, hukiri mambo yasiyokuwapo kana kwamba yametokea, hufanya sasa (Warumi 4:17-21).
II.            NAMNA ZA UKIRI WA IMANI
Kukiri ni kukubaliana na kitu fulani na kukisema (Amos 3:3)
A.    Kumkiri Yesu (Warumi 10:9-10)
·         Kukubaliana na Yesu alivyo na kumsema kama alivyo
·         Kukubaliana na kazi ya Yesu aliyoifanya na kuisema
B.    Kukiri dhambi (1Yohana 1:6-8)
·         Kukubaliana na Mungu kwamba umetenda dhambi na kusema mbele yake.
·         Kukubali kwamba umemkosea mtu na kusema (Yakobo 5:8)
C.    Kukiri Neno (Waebrania 13:5-6)
·         Kukubaliana na neno la Mungu linavyosema na kusema kama linavyosema, kuwa na uhakika moyoni linaenda kudhihirika kama lilivyosema.
·         Kukubaliana na neno na kulisema 1. Mbele za Mungu 2. Mbele za mazingira 3. Mbele za shetani, kisha kuwa na uhakika linatokea.
D.    Kukiri habari njema (Marko 16:15-17)
·         Yesu alisema twende ulimwenguni mwote tukahubiri kwa kila kiumbe, kuhubiri ni kukiri neno kwa wenye dhambi na kuwa na uhakika linaenda kutenda  1. Kuponya 2. Kuokoa 3. Kukomboa
E.    Kukiri kazi ya Yesu
·         Kusema na kuwa na uhakika
1.    Yesu alifanya nini mbele za Mungu kwaajili yako 2Wakorintho 5:18, Wakolosai 1:20
2.    Yesu alifanya nini mbele za Shetani kwaajili yako Wakolosai 2:15, 1Yohana 3:8
3.    Wewe ni nani katika Kristo, 2Wakorintho 5:20
4.    Una kitu gani katika Yesu Warumi 5:17

No comments:

Post a Comment