Imani
na Kufunga
Yesu
aliwaambia wanafunzi wake, namna hii haiwezekani ila kwa kusali na
kufunga (Mathayo 17:21). Hapa alionyesha kuna namna ya pepo au
matatizo yanayo ondoka kwa imani maalum, inayozaliwa mtu akifunga.
Kufunga
na kuomba kunaongeza imani na ujasiri wa kuachilia nguvu iliyopo
rohoni . Kufunga ni kichocheo cha imani na udhihirisho wa karama za
rohoni. Wakati wa kufunga yafuatayo hutokea:
1. Roho ya mtu huwa
nyepesi kufahamu miendo ya Roho Mtakatifu
2. Akili hutiwa nuru na kuwa makini, umakini (concentration) unaongezeka.
2. Akili hutiwa nuru na kuwa makini, umakini (concentration) unaongezeka.
3.Ulimwengu wa roho
huwa wazi zaidi, hivyo kupokea mambo ya rohoni kirahisi, ikiwepo
imani na ufahamu.
4. Nafsi ya mfungaji hutiishwa chini ya Mungu,
hunyenyekezwa, hivyo kumfanya Mungu ainuliwe katika maisha ya
mfungaji.
Wakati
wa kufunga huambatana na kusoma sana Neno, kuabudu na kunena kwa
lugha muda mrefu, pia kuamuru vitu unavyoviona kwa imani vitokee. Kwa
kufanya hivi imani kuu inaweza kudhiirika na kutenda makuu.
Ngao
ya Imani
Katika
Waefeso 6:16 maandiko yanasema, “zaidi
ya yote mkiitwaa ngao ya imani ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima
mishale yote yenye moto ya yule mwovu,”
Hapa imani imetajwa kama silaha ikifananishwa na ngao. Ngao hii
imeonekana kuwa na uwezo wa kuzuia mishale ya moto ya Shetani.
Mishale hii bila shaka ni hila zote ambazo Shetani huzitumia katika
fikra au mawazo ili kumtoa mtu katika hali ya kuamini kwa kumtumaini
Mungu kudhihirisha alichosema. Tofauti na karama ya imani ngao ya
imani yatupasa kuwa nayo wakai wote.
Wakati
fulani nilikuwa katika jaribu, wazo likanijia lisemalo “Mungu
hakupendi angekuwa anakupenda yasingekupata haya” Wazo hili
lilikuwa kama mshale, moto wake ulikuwa ni hali ya mashaka na
wasiwasi kuhusu upendo wa Mungu kwangu. Niliweza kupinga wazo hilo
kwa imani katika pendo la Mungu kama maandiko yanavyoonyesha,
alinipenda na kumtoa Yesu kwaajili yangu ili nipate uzima (1Yohana
4:9). Hatutikisiki katika imani zetu kwa Mungu kwa kuwa tunalijua
pendo
lake kwetu na kuliamini. Wazo lolote lililo na hofu ndani yake ni
mfano wa mshale wenye moto, lazima imani katika uaminifu
wa Mungu kwa yale aliyosema ilizuie. Mshale
ni mfano wa wazo la kishetani, moto
ni mfano wa woga au hofu inayokuja na wazo hilo. Ngao ya imani
hufanya kazi kwa njia ya kutumainia uaminifu
na upendo
wa Mungu, Biblia inasema, “…uaminifu
wake ni ngao na kigao”
(Zaburi 91:4). Pia Biblia inasema, “Nasi
tumelifahamu pendo alilonalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini…”
(1Yohana 4:16). Shetani aletapo wazo kama mshale lisemalo, “ugonjwa
huu utakuua” , kisha
moto wa woga na kukata tama ukaanza kuwaka, imani zetu hulipinga wazo
hilo kama ngao kwa kuwa tunajua Mungu aliyesema kwa kupigwa kwa Yesu
tumepona ni mwaminifu na dhahiri, pia anatupenda kiasi cha
kudhihirisha uponyaji wake kwetu.
No comments:
Post a Comment