Skandalidzo
“Maneno hayo
nimewaambia, msije mkachukizwa”
(Yohana
16:1)
Neno kuchukizwa katika andiko hili kwa Kiyunani ni, “Skandalidzo”. Tafsiri yake ni: kujikwaa, Kusababisha mtu
kuanza kutomwamini mtu aliyemwamini na kumtegemea.
Mathayo 24:10 inasema, “Ndipo
wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana na kuchukiana” Neno kujikwaa hapa
ni hilo tunalolizungumzia, Tulilolitaja hapo juu.
Mkakati mmoja wa kishetani kwa mtu wa Mungu, hasa mtumishi ni
kusababisha watu anaowahudumia wachukizwe naye.
Yesu katika andiko la Yohana 16:1, alionyesha kwamba
atakapoondoka yatatokea matatizo kwa wanafunzi, ambayo yangeweza kuwafanya
wachukizwe naye. Matatizo haya yangemtengenezea Yesu ‘skendo’ kwamba amewatuma
kuhubiri na bado wanatengwa na masinagogi nk.
Hii bila shaka ingeweza kufanya wanafunzi wachukizwe na Yesu. Mmoja
ambaye angeweza kuleta matatizo haya, bila shaka angekuwa ni Shetani ili
kumpaka matope Yesu, kum-“skandalidzo” kumfanya achukize. Aonekane hafai.
Ndicho anachokifanya leo Shetani. Anachochea ‘skendo’ hasa kwa
watu wa Mungu ili wachukize. Wakichukiza maneno yao na huduma wanazofanya
zitakosa kibali. Hatimaye wanakosa
ujasiri mbele za watu na hata mbele za Mungu. Hali hii ikitokea wasiposaidiwa
huduma inaweza kulala au hata kufa.
LEO TAMKA NEEMA YA KUOKOLEWA TOKA KATIKA SKENDO, KWA MTUMISHI YEYOTE
ANAYEKUHUDUMIA. IKIWA SKENDO HIYO NI YA KWELI AU YA UONGO. JIOMBEE NAFSI YAKO USIWE
MMOJA WAPO WA CHOMBO CHA SHETANI CHA KUMFANYA MTU WA MUNGU ACHUKIZE, HATA KUUA
HUDUMA YAKE. FURAHIA MAMBO MEMA YA WATUMISHI, WATIE MOYO WAKIFANYA VIZURI,
USISUBIRI WAKOSEE NA KUANZA KULAUMU.
No comments:
Post a Comment