Roho
Yangu Inatoka
Siku moja asubuhi kama
saa kumi na mbili niliamka toka kitandani na kukaa. Nikasikia sauti ikisema
nyuma yangu, “Leo unatoka duniani” Niliposikia
sauti hii, ilinijia hali moyoni ya kujihurumia nafsi yangu na kusikitika
masikitiko ambayo hayaelezeki. Nilianza
kububujikwa na machozi huku nikirudi kitandani.
Nilipolala tu, kitandani hazikupita hata dakika mbili nikatoka katika
mwili wangu. Nikajikuta nimesimama
pembeni ya kitanda! Kitu cha ajabu nilikuwa nimesimama na hapo hapo najiona tena
nimelala. Nilikuwa namwona ‘mimi’ mwingine amelala kitandani! Nilishangaa
kujiona nimesimama wakati huo huo namwona mtu mwingine kama
mimi kalala kitandani. Kumbe nilikuwa nimetoka katika mwili, nimekufa. Niliyemwona mwingine kalala ni mwili wangu.
Mimi halisi nilikuwa nimesimama.
Shimo Lafunguka
Ghafla pembeni yangu kwa chini nikaona
lango limefunguka, kumbe ni shimo refu sana
lenyekutisha. Niliona nisogee karibu na
shimo hilo
niweze kuona urefu wake. Wakati
ninasogea nilivutwa na nguvu ya ajabu ambayo siwezi kuielezea. Nilianza kuvutwa
chini kama vile ninabembea huku
nashangaa. Nilifika chini sana, lakini haikuwa ni
mwisho wa shimo. Ilikuwa niko mbali sana,
nikagundua sikuwa ndani ya shimo nilikuwa ndani ya ulimwengu mwingine!
Nikaanza kulia kilio ambacho sijawahi kulia. Moyoni nilianza kupatwa na hali ya kuona
nahitaji atokee mtu anisaidie. Nilianza
kukimbia kuelekea mashariki, huku nikilia kilio ambacho hakina maelezo.
Nikawaza nikimbilie mashariki labda nitapata mtu wa kunisaidia. Nilikuwa mwepesi mwenye kasi kubwa niliweza
kuruka angani. Chini yangu kulikuwa na
mngurumo unaotisha. Nikapita kwenda magharibi, kusini na kaskazini. Nilipotoka
kusini nilirudi huku nikikimbia kwa kukata tamaa, nilirudi mahali nilipoingilia
huku nimekata tamaa ya kupata mtu wa kunisaidia. Nikaanza kulia sana kama muda wa nusu
saa.
Ninaokolewa
Toka Shimoni Kuzimu
Nikasikia wazo! Au sauti sijui!
Ikisema moyoni mwangu, “angalia juu”. Nikainua macho yangu juu, nikamwona mtu yupo
juu sana
ng’ambo nyingine. Alinitazama kwa
kunihurumia huku akinyosha mikono yake miwili kwangu. Nilipoona mikono ile niliacha kulia na kuanza
kujiandaa kumrukia ingawa alikuwa juu sana. Moyoni niliazimia lazima nimshike mikono na nikimshika
nitamshika kwa nguvu kiasi kwamba ningeweza kurudi naye shimoni, ila asingeweza
kuniachia. Nikaruka nilikuwa mwepesi
nikaenda juu mpaka alipo nikaingiza mikono yangu katika mikono yake. Nilipoiingiza mikono akanipokea, akanichukua
haraka na kuniweka mkono wake wa kuume.
Akaniangalia kwa sekunde! Sura yake sikuishika, akapotea. Kisha yakatokea maandishi hewani pale
alipokuwa amesimama, “YESU KRISTO”.
Hakuwa mwembamba wala mnene, alikuwa na kimo cha wastani.
Nimerudi
Mwilini
Baada ya hapo nikajikuta nimeingia
katika mwili wangu kitandani, nikakaa. Ghafla nikasikia sauti nyuma yangu ikisema, “Wewe umetokaje huko, huko wakienda huwa
hawatoki, wewe umetokaje? Sasa jiandae utarudi tena huko.” Niliijibu ile
sauti na kusema kufa nakubali kufa, lakini kule shimoni sirudi nitaenda na
Yesu. Sauti ile iliendelea kunisumbua,
ikasema tena, “Ulitokaje huko jiandae
utarudi tena huko” Nikasema sitarudi
tena huko naenda na Yesu, sauti ikanyamaza.
Ni Amina na Kweli. Neema ya Kristo izidi Kutuwezesha Kumjua YEYE Aliye wa KWELI.
ReplyDeleteAsante!
ReplyDelete