Friday, July 4, 2014

MAANA YA IMANI -1



TAFSIRI YA IMANI
Katika somo hili utajifunza imani ni nini na mazingira ya utendaji wake. Litakusaidia kufungulia imani ambayo tayari unayo ikiwa umempa Yesu maisha yako. Maandiko yanasema:
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo yasiyo onekana(Waebrania 11:1)
Katika andiko hili tunaona imani ikitafsiriwa maeneo katika mawili:
1.       Kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo
2.        Bayana ya mambo yasiyo onekana
KUWA NA HAKIKA
Kama ilivyoandikwa, imani ni kuwa na hakika. Tafsiri nzuri ya  maneno haya ni “Imani ni kuwa na uhalisi wa sasa”. Neno la Kiyunani lionyeshalo uhakika katika andiko hili ni hupostasis. Maana ya neno hili ni “kitu kinachowekwa chini ya kitu kingine”, ni mfano wa msingi uliobeba kitu, kama vile nyumba. Msingi wa nyumba unaweza ukawa hauonekani, lakini ni uhakika wa nyumba kusimama, ndiyo nyumba,  ni uhalisi wa nyumba!
Neno hili hupostasis pia limetumika Waebrania 1:3  Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake…” Nafsi yake Mungu haionekani, lakini ndio uhakika na uhalisi wa sasa wa Yesu anaye onekana, Yesu ni chapa, ni mwonekano wa nje wa Mungu asiye onekana aliye uhalisi wa Yesu anayeonekana. Uhakika wa Yesu anayeonekana ni “nafsi yake” asiye onekana.
Imani ni uhalisi unaobeba sasa, mambo yatarajiwayo kuonekana baadaye. Unayaona kwa uhalisi sasa na kuyashika mambo yatarajiwayo kuonekana au kudhihirika baadaye.
MAMBO YATARAJIWAYO
Haya ni mambo tunayotarajia kutokea wazi ambayo yameshikwa na imani au yamekuwa halisi tayari ndani yetu. Hakuna msingi unao beba kitu kinachotarajiwa kutokea ila imani. Kwa mfano mguu ukiuma na ukawa unatarajia kuona udhihirisho wa kupona, imani ni uhalisi wa sasa ndani yako, unaokupa hakikisho sasa kwamba unalo jambo unalo tarajia kuliona, yaani mguu kupona. Msingi wa matarajio ya kupona mguu wako ni uhalisi wa sasa uuonao ndani yako kuhusu uzima wa mguu.
Sehemu hii ya kwanza tumeangalia Imani inabeba au inashika mambo unayotarajia kupokea. Inayashika kabla hayajaonekana.  Kabla hujapokea jambo ambalo unatarajia kuliona likidhihirika, imani ni uhakika au msingi wa jambo hilo litarajiwalo. Usipojenga msingi huu usioonekana hutaliona kwa nje likionekana.
Sehemu itakayofuata tutaangali BAYANA YA YASIYOONEKANA.

1 comment: