Sunday, July 13, 2014

Jikumbushe Tena Kuhusu Imani




IMANI NI NINI? (Waebrania 11:1), “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo…”.  Kwa maneno mengine tafsiri hii inasema, “ Basi imani ni uhakika, ni hati miliki ya vitu tunavyovitarajia vidhihirike”. Imani ni hati miliki ya moyoni, unayo hata kama mwilini huoni ulichomiliki, lakini ndani tayari unacho na una uhakika wa kuona udhihirisho wa kutokea kwake kwa nje. Ukiwa na hati ya nyumba unauhakika kuwa unayo nyumba hiyo hata kama huioni.

A.    Imani ni kumiliki sasa mambo yanayoenda kudhihirika kwa kuonekana.
B.    Imani ni kupokea sasa kitu kitakachoonekena baadaye au muda mfupi ujao.
C.    Imani ni msingi wa mambo yatakayodhihirika. Bila msingi huo hayadhiriki.
D.    Kabla ya jambo kudhihirika uhakika wa udhihirisho wake ni Neno la Mungu. Neno hili huzaa uhakika huo moyoni, huwa ni msingi wa kudhihirisha litarajiwalo.
E.    Imani ni uhakika wa moyoni unaopokea sasa na kujenga tumaini akilini la kuona udhihirisho wakati ujao.
F.    Kabla ya udhihirisho imani ya moyoni au uhakika wa moyoni, huomba, hushukuru, husifu, hukiri mambo yasiyokuwapo kana kwamba yametokea, hufanya sasa (Warumi 4:17-21).
G.    Matendo haya yaani kuomba, kushukuru, kukiri nk ni kuamini.  Imani ni jina, imani hukaa moyoni, kuamini ni tendo hufanyika mwilini kuleta udhihirisho.

Maswali
1. Kwa Maneno yako Mwenyewe Elezea Maana ya Imani?
2. Kuna mahusiano gani kati ya imani, kuamini na yatarajiwayo?
3. Utafanyaje kwenye uhitaji ulionao ili uamini na kudhihirisha yatarajiwayo?

No comments:

Post a Comment