Kudhibiti Hasira
Wote tuna hasira, hii ni nguvu iliyopo ndani yetu, Hata hivyo
inapaswa idhibitiwe ili tusitende dhambi kwa hiyo. Hasira ipo kwetu ila
yatupasa tuiweze.
“Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vyote vifaavyo; vitu
vyote vi halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya uwezo wa kitu chochote.”
(1Wakorintho 6:12)
1. Usikae na Vidonda
Shughulikia vidonda haraka, ulivyoumizwa, hasa vya wakati wa
utoto. Mweleze Mungu jinsi ulivyoumia kisha mtwishe fadhaa hiyo kwa imani na
kuacha kuibeba, mwachie yeye abebe uchungu au fadhaa hiyo. Ukidumu kufanya
hivyo kwa muda utapona na hasira inayotokana na uchungu wa nyuma itaisha (1Pet
5:7).
2. Usiseme Mpaka
Ufikiri
Jambo la kukasirisha, ambalo linaweza kukufanya upitilize
kusema au kutenda, likitokea, usiseme chochote mpaka kwanza ujiweze kwa
kufikiri (Yakobo 1:19). Hasira huleta
hali ya kutenda au kusema jambo bila kufikiri. Hivyo unapokasirika lazima
ushike kufikiri kwako kusipote. Namna moja wapo ya kufanya ni kuondoka kwa muda
eneo husika na kukaa sehemu tulivu huku
mwili wako umetulia. Hii itakusaidia kufikiri kabla hujasema au kutenda
jambo, pia itakuwezesha kujitenga na ugomvi (Mithali 20:3).
3.Omba Hekima
Hekima inaweza kuombwa kwa jina la Yesu (Yohana 16:23, Yakobo
1:15). Hekima ya Mungu inayo mambo mazuri, ina matunda mema (Yakobo 3:17).
Ikaapo moyoni inaweza kukusaidia kufanya jambo jema la kudhibiti hasira, hekima
inaweza kufanya jambo lolote jema ndani yako ikiwemo kutuliza hasira.
4. Jizuie Kuumiza
Mara nyingi moyo wa hasira hupenda
kuumiza, Hasa kama chanzo cha hasira hiyo ni kuumizwa. Ukipenda kuumiza utaumia
mwenyewe kwanza. Ukitaka kuumiza ukuta au hata mtu kwa kumpiga ngumi, maumivu
yatatokea mkononi mwako kwanza! Kadhalika ukitamka neno baya la kuumiza
unajiumiza mwenyewe kwanza. Ukifurahisha wengine utafurahi wewe kwanza. Huwezi
shughulikia hasira ukiwa unaumiza watu! Haitaisha. Ukitenda mema kwa watu
utaanza kupona wewe kabla hata ya wao ! (Mathayo
7:12).
5. Vua Hasira
Unaweza kutenda lolote kwa jina la
Yesu (Wakolosai 3:17). Unaweza kuivua roho ya hasira, hasira ambayo si ya
kawaida inaweza kuwa ni roho, unaivua kwa jina la Yesu (Waefeso 4:23-24). Ivue
katika hisia zako za nafsi kwa jina la Yesu.
Hasira iletayo dhambi waweza ivua kwa jina la Yesu. Ongea nayo kama
roho.
6. Nena kwa Lugha
Ikiwa unanena kwa lugha tumia muda
mrefu kunena. Kunena kwa lugha
kunakujenga katika mambo mbalimbali. Kunakufanya imara roho yako. Kunaweza
kukusaidia kuidhibiti hasira. Ukasirikapo mara nyingine nenda mbele za Mungu,
msifu na kunena kwa lugha, hisia mbaya za hasira zitaisha furaha itatokea!
HASIRA IPO IWEKEE
MPAKA
Thanks Pastor. Wengi tusaidika kwa hili pia. Bwana Azidi Kukutumia.
ReplyDelete