Tuesday, December 2, 2014

Wito wa Roho Mtakatifu 2



KAZI NYINGINE ZA ROHO MTAKATIFU
I. Roho anatuwezesha kuomba na kutumika kwa usahihi (Warumi 8:26-28)
·   Tunaomba ila si kwa usahihi wakati wote, huu ni udhaifu. Hatuwezi kuomba kwa maneno sahihi (articulate speech) bila Roho Mtakatifu.
·         Roho hutusaidia udhaifu huu kwa kuwa pembeni nasi na kutupa maneno ya kuomba.
·         Si kuomba tu, hata kuimba, kufundisha na kuhubiri. Hatujui kufanya huduma kama itupasavyo huu ni udhaifu. Roho hutusaidia udhaifu wetu, tumtegemee.
II.           Anatia nguvu kanisa na huduma zote hasa tano kwa karama tisa.
III.          Mungu ametumiliki kwa njia ya Roho
·         Roho ni uhakikisho wa wakati wote katika ulimwengu wa Roho kwamba sisi ni mali ya Mungu:
1.   Ni muhuri (waefeso 4:30)
2.   Arabuni (Waefeso 1:14)
·         Arabuni maana yake ni ‘deposit’ Mungu ametupa uzima wake wa milele, kwa njia ya Yesu tutaishi naye milele. Roho aliyendani yetu anaonyesha uhakikisho huo.  Muhuri ni ishara au alama ya kumilikiwa na Mungu. Roho nadi yetu ni alama ya kuonyesha sisi tu mali ya Mungu.
IV.         Roho anatufundisha yote
·         Yohana 2:27, andiko hili laonyesha ‘mafuta’ yaani Roho Mtakatifu anatufundisha mambo yote! Si ya kiroho tu, mfano:
-      Kufanya biashara
-      Kusoma
-      Kuomba
-      Kupigana vita vya kiroho
-      Kuheshimu wa zazi
-      Kula vizuri
-      Kufunga
-      Kufanya uinjilisti
-      Kulea watoto
-      Kuvaa vizuri nk 
·         Yeye ni Msaidizi wa maisha yetu yote, kama alivyokuwa Yesu kwa ulimwengu. Alopokuwa duniani, aliwaponya watu, aliwapa chakula, alienda kwenye msiba, alienda kwenye mazishi na kufufua wafu nk.
V.           Roho na huduma ya kuufikia ulimwengu
·         Mitume walifanya na kuamua mambo wakiwa pamoja na Roho Mtakatifu (Matendo 15:26). Roho Mtakatifu alikuwa kama Mwenzao aliyepembeni yao kuwasaidia. Moja ya namna ya kufanya kazi na Roho ni kujua kwamba yupo, ni kumtambua. Baada ya hapo kumshirikisha mambo yetu, kwa kuongea naye, atatusaidia!
·         Roho ni shahidi kwa ulimwengu (Yohana 16:13-15)
-      Anashuhudia kwa kuwaonyesha watu dhambi ya kutomwamini Yesu.
-      Wanahesabiwa  Haki kwa njia ya imani ya Yesu
-      Watahukumiwa Yesu

  Roho alihusika katika uinjilisti wa watumishi wafuatao, soma maandiko haya kisha elezea alihusikaje?

I.             Petro
(a)  Matendo 4:5-8)
(b)  Matendo 10:17-19
II.           Setano
(a)  Matendo 6:8-10)
III.          Filipo
(a)  Matendo 8:4-8
(b)  Matendo 8:26-40

No comments:

Post a Comment