Wednesday, December 3, 2014

Ushirika na Roho Mtakatifu



JENGA USHIRIKA NA ROHO MTAKATIFU
Kabla ya kufanya huduma yoyote, ni vema kujenga ushirika na Roho Mtakatifu, yeye ni Roho wa ushirika (2Wakorintho 13:14), (Yohana 16:13-15).
Mambo yafuatayo yatakudaidia  kujenga ushirika na Roho Mtakatifu:
I.             Tambua yupo na wewe wakati wote. Hata kama hujisikii.
II.           Kutana naye kwenye Neno la Mungu. Neno ni ‘kituo cha makutano’ na Roho Mtakatifu, sema  ….. “ninaposoma neno hili, leo nipo na wewe Roho Mtakatifu” . Ongea naye kama ‘mtu’ aliye pembeni yako anayekusikiliza.
III.          Jizoeshe ajifunue kwako kupitia Neno la Mungu.
IV.         Onyesha huwezi, kwa kumwambia, “Roho bila wewe siwezi” (Yohana 15:5).
V.           Jizoeshe kuikiri nafsi na uzuri wa Yesu maishani mwako Roho atatokea. Yesu akipambwa na kusema vizuri, Roho Mtakatifu hujidhihirisha. Sema vitu vifuatavyo vya Yesu:
·         Damu ya Yesu
·         Jina la Yesu
·         Yesu mwenyewe
VI.         Ili kudumisha ushirika usimfanyie yafuatayo
1.   Usimzimishe (1Wathesalonike 5:19)
                      Chochea utendaji wake ndani yako
Mfano
-      Ukianza kunena endelea kila siku, jijenge kwa Roho Mtakatifu kwa kunena kwa lugha.
-      Ukianza kusoma Neno na kujifunza kwa Roho, fanya kila siku
-      Ukiishi kwa upendo kinyume na mwili endelea
-      Ukitafakari na kufunuliwa maandiko tafakari kila siku
-      Ukiomba na kuabudu endelea
-      Ukiona udhihirisho wa Roho binafsi endelea usizimishe
-      Usiache kutumia karama na vipawa vya Kiungu ulivyonavyo
Kumzimisha Roho hufungulia mlango wa kumuhuzunisha.
2.   Usimuhuzunishe (Isaya 63:10), (Waefeso 4:30)
Roho anahuzunishwa kwa uasi, dhambi ni uasi. Wakati wote uwe kinyume na dhambi na matendo ya mwili. Kumuhuzunisha Roho hufungua mlango wa kumpinga.
3.   Usimpinge (Matendo 7:51)
·         Kumpinga (antipipto) ni kukataa msukumo wake kufanya jambo, kama vile mbuzi au punda akataavyo kutembea akiamua. Roho anapokukataza kufanya jambo fulani, ukilazimisha maana yake unampinga. Hatua hii hufungua mlango wa kumfanyia jeuri.
4.   Usimfanyie jeuri (enubrizo)
Kumfanyia jeuri ni sawa na kumtukana, sio rahisi mtu afikie kiwango hiki! Lakini ukiruhusu kumzimisha utaruhusu kumhuzunisha, baada ya kumuhuznunisha utampinga, baada ya kumpinga utamfanyia jeuri hii ni hali mbaya kuliko zote ambayo mtu anaweza kufikia na kuvunja ushirika na Roho Mtakatifu.

Ushirika mkubwa na Roho unajengwa kwa KUTOMZIMISHA. Kufanya mambo ya Kimungu wakati wote: Kuomba, kusoma Neno, kufunga, kusifu na kuabudu, kusamehe, kupenda, kukiri Neno nk. Ukiwa katika hali hii utaweza kufanya huduma ya kuufikia ulimwengu kwa ROHO MTAKATIFU.


No comments:

Post a Comment