Wednesday, November 26, 2014

Huduma za Kanisa


      Huduma Moja kwa Wote Wakiwa Wote

Kanisa kama mwili mmoja wa Yesu, lina huduma. Ingawa ndani yake kuna watu wenye huduma mbalimbali. Huduma hizi zinaonekana katika huduma  tano na huduma za masaidiano. Hata hivyo ukilitazama kanisa lote kama mwili lina huduma, inayotendwa na lote kama mwili mmoja.

A.   Kumuhudumia Mungu
Mungu ana uhitaji ndani yake, anataka ahudumiwe kwa sifa, shukrani na kuabudu (Matendo 13:1-3). Katika andiko hili, waalimu na manabii walimtolea Bwana ibada na kufunga, walimuhudumia. Sisi binafsi na kama mwili wa Kristo tuna huduma ya kumuhudumia Mungu. Kabla ya kuhudumiana sisi kwa sisi na kuuhudumia ulimwengu ni lazima kumuhudumia Mungu kwa sifa na shukrani.
B.   Kuhudumiana
1Wakorintho 12, inaonyesha kanisa ni mwili. Kiungo kimoja kikiumia vyote huumia pamoja nacho. Wajibu wa mwili mzima upo kwaajili ya kiungo kimoja. Viungo vyote vinawajibu wa kutunza kiungo kimoja. Viungo yapasa vitunzane hii ni huduma ya sisi kwa sisi, kwa rehema, kukarimu,usimamini, maombezi, kufanya wanafunzi, kuchungwa, kufundishwa, kufarijiwa, kujengwa, kuonywa nk. Kumhudumia Mungu vizuri kisha kuhudumiana sisi kwa sisi, huufanya mwili uwe na nguvu ya kuuhudumia ulimwengu.
C.   Kuhudumia Ulimwengu
Kanisa zima tuna wajibu wa kuhudumia ulimwengu. Yesu alisema, “Enendeni..." (Marko 16:15-17). Wote yatupasa kwenda ulimwenguni huu ni wito wa kanisa. Kanisa lisiloufikia ulimwengu limepoteza lengo (shabaha) ‘limetenda dhambi’, kutenda dhambi ni kupoteza shabaha fulani ya kiungu. Kazi ya kanisa lote ni kuhubiri injili na kufanya wanafunzi (wafuasi watakao kuwa kama Yesu).
Kuhubiri + kufanya wanafunzi = huduma ya kanisa kwa dunia.
v  Kuhudumia ulimwengu kwa msingi ni kuufikia kwa injili.
v  Huduma zote tano na za masaidiano hatma yake moja kuu ni mwili wote uwe na ‘afya’ ya kuweza kuufikia ulimwengu.

No comments:

Post a Comment